Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UCHAMBUZI WA PRIVADINHO KUHUSU MECHI YA YANGA NA MAMELODI


Mamelodi leo walionesha kitu ambacho mara nyingi wanakionesha Brighton ( kwenye build up ) kipi hiko ?Kukuvuta uende kuwafanyia pressing ( Baiting the press ) na kwanini hivyo ?

1: Ni kwamba wanapasiana taratibu nyuma pasi fupi fupi dhamira yao uende ukawafanyie pressing ili space ifunguke nyuma yako washambulie nyuma ya kiungo chako , pasi mbili au tatu wanakusalimia

2: Wanakuwa mabeki wawili nyuma , viungo wawili mbele yao huku fullbacks wakiwa wanatanua uwanja kwenye mstari wa mmoja na viungo wawili , huku GK anakuwa kama option ya ziada wakitaka pasi ya mbele

Lakini Yanga wao wakasema " No thank you " huo mpira kaeni nao huko kwenu hatuji kufanya pressing , Yanga walitengeneza midblock nzuri ya 4-4-2 ( walikabia katikati zaidi na wala sio chini wala juu sana ) kuwanyima space za ndani ya Mamelodi jumlisha kazi nzuri ya Maxi na Musonda kwenye ku track back kuhakikisha fullbacks wao wasiwe wazi peke yao . Game Plan

Kwa kipindi cha kwanza tu pekee ilihitaji hivi vitu viwili goli lipatikane

1: Makosa makubwa ya kiulinzi kwa timu zote mbili
2: Ubora wa mchezaji mmoja kuamua ( individual brilliance )

Kipindi cha pili kuna muda kama wa dakika 20 au 15 fulani hivi , timu zote mbili ziliamua kufunguka na kupishana hapo spaces zilianza kufunguka , runners wakaanza kupata spaces , pasi za mbele zilianza kuonekana , kilichokosekana :-

1: Mamelodi pasi yao ya mwisho ilikosekana
2: Yanga maamuzi sahihi , either pasi au umaliziaji

kwenye uzuiaji timu zote zilikuwa tofauti kwenye muundo wao

Mamelodi walichagua kukabia juu hasa pale wakipoteza mpira ( counter pressing )

Yanga kufunga spaces wakiwa ndani : na wote ( Mamelodi na Yanga walifanikiwa kwenye mipango yao )


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC