Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA INA KILA SABABU YA KUITOA AL AHLY

Na Prince Hoza


MWISHO wa Al Ahly umefika naweza kusema hivyo, mpira umebadilika sana hapa Afrika na tumejionea kwenye michuano iliyomalizika ya mataifa Afrika, AFCON iliyofanyika nchini Ivory Coast ambapo timu maarufu ziliambulia patupu. 

Lakini pia michuano hiyo tumeshuhudia miamba ya kutoka Afrika kaskazini, kwa maana timu za Kiarabu kuondoshwa mapema, mataifa makubwa kama ya Morocco, Algeria, Tunisia na Misri zilishindwa kupenya. 

Kushindwa kwa mataifa hayo, kulizifanya mataifa yasiyo na umaarufu kuibuka, hivyo ndivyo ilivyo kwa upande wa vilabu katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika na kombe la Shirikisho. 

Katika Ligi ya mabingwa, safari hii mataifa ya Waarabu hayajafua dafu na kujikuta yakiondoshwa mapema, Al Ahly na Esperance ya Tunisia ndio timu pekee zilizofanikiwa kuingia robo fainali, na mwenendo wao si mzuri.

Vilabu kama vya Pyramids ya Misri, Wydad Casablanca ya Morocco na CR Belouizdad ya Algeria ziliishia makundi. 

Sio kawaida kwa mataifa ya kiarabu kuondoshwa mapema, lakini utawala wao kwenye soka umeonekana kuyumba na kama si kuondoshwa kabisa. 

Ni maajabu makubwa kwa taifa la Tanzania kuingiza timu mbili robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika, Simba SC na Yanga SC zote zimefanikiwa kutinga hatua hiyo.

Miamba hiyo imeungana na TP Mazembe ya DR Congo, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na Petro de Luanda ya Angola. 

Nyingine ni Esperance ya Tunisia, Al Ahly ya Misri na Asec Mimosas ya Ivory Coast, kama ilivyotokea kwenye michuano ya AFCON kule Ivory Coast ambapo mataifa ya Kiarabu ilipoanguka vibaya. 

Mataifa kama ya Algeria, Morocco, Maurtania, Tunisia na Misri ambapo yaliishia njiani, Ivory Coast na Nigeria zilicheza fainali na ukawa mwisho wa Waarabu. 

Al Ahly itakutana na Simba katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, nauona mwisho wa Ahly kama Simba itapambana kufa na kupona, Simba wasichukulie kama wanakutana na mkubwa wa soka barani Afrika, waichukulie kama Ahly timu ya kawaida na wanaweza kuiondosha. 

Wakati miamba hiyo inakwenda kukutana, rekodi inaonyesha timu hizo zimekutana mara sita katika kipindi cha misimu minne huku zote zikiwa sawa, Ahly imeshinda mara mbili na Simba pia mara mbili. 

Miamba hiyo imetoka sare mara mbili, rekodi inawabeba Ahly kwa kuifunga Simba mabao mengi zaidi.

Na pia imewahi kuiondosha Simba kwa mujibu wa sheria ya mabao ya kufunga na kufungwa, miamba hiyo ilikutana kwa mara ya 5 ilishinda mabao 5-0 na katika mchezo wa marudiano Simba ilishinda 1-0 ikumbukwe ilikuwa kwenye hatua ya makundi, pia msimu wa 2020/2021 zilikutana tena Simba ikishinda 1-0 mjini Dar es Salaam na ziliporudiana Cairo, Ahly ilishinda 1-0. Na mara nyingine zilikutana katika michuano ya African Football League (AFL) ambapo Ahly iliiondosha Simba kwa sheria ya magoli ya kufunga na kufungwa. Zilipokutana jijini Dar es Salaam zilitoka sare 2-2 na zilipokutana tena mjini Cairo zilitoka sare ya 1-1, ni wakati wa Simba kuiondosha nje Ahly, timu hizo zimeshakutana msimu wa  2018/2019.

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC