Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MOHAMED CHUMA ALIKUWA BEKI WA KATI TAIFA STARS


MOHAMED Ali Chuma alikuwa ni mmoja wa mabeki wazuri kuwahi kutokea katika nchi hii ya Tanzania. Chuma alikuwa anamudu kucheza namba 3, 4, 5, na 6.

Chuma alizaliwa katika kijiji cha Naumbu mkoani Mtwara 1943. Chuma alianza kung' ara katika michuano ya Sunlight Cup 1966 na baadaye katika Taifa Cup 1970/1973. 

Chuma aling' ara pamoja na akina Sembwana Behewa, Mweri Simba, Abdallah Luo na Omary Zimbwe kutoka mkoani Tanga, akina Shiwa Lyambiko, Kasim Manga, Adam Sabu kutoka Morogoro.

Chuma alikuwa na uwezo mkubwa wa kukaba winga au mshambuliaji hatari.
Chuma katika timu ya Taifa Stars mwaka 1973 alicheza soka la hali ya juu na washambuliaji wengi wa Kenya kama akina Agonda Tukiyo au Allan Thigo walikuwa wanamuogopa na hata Timothy Aiyeko wa Uganda alikuwa anamhofia Chuma anapokutana nae.

Chuma alikuwa ni mchezaji wa kiwango cha juu na ingekuwa miaka hii ya sasa Chuma angekuwa anaicheza soka barani Ulaya. Chuma miaka ya 1967 alikuwa anaichezea Beach Boys na akina Juma Gayo Mandoa, Musa Okelo, Issa Pele, Muhaji Mukhi na wengineo. 

Chuma alikuwa anang' a sana anapokuwa na klabu yake ya Nyota FC ya Mtwara akicheza na akina Abdurahman Zimbo, Iddi Pazi, Ibrahim Shomar, Iddi Dogoa na Bakari Bomba.

Wengine ni Denis Mrope, Isaya Namajojo, Mohamed Mkandinga, Said nyingema, Rashid Hanzuruni, Juma Kibonge, Amin Buljji, Mzee Kwasa, Joseph Agostino na Hamisi Masika. 

Chuma pia katika timu ya mkoa wa Mtwara katika kombe la Taifa, Taifa Cup alicheza na akina Haji Masoud, Hamim Mawazo, Shomar Seleman, Juma Mkambi "General" na Seleman Omary. 

Chuma 1974 alikuwepo katika timu iliyochukua kombe la Chalenji akiwa na akina Omary Mahohamed, Chuma alikuwepo katika timu ya taifa, Taifa Stars 1973 iliyoshiriki mechi za kufuzu za AFKON akiwa na kocha Shabani Marijani.

Na nyota wangine akina Sunday Manara, Willy Mwaijibe, Jumanne Hassan, Haidar Abeid, Abdallah Kibaden, Mustafa Kasimu, Shabani Baraza, Omary Zimbwe, Mwabuda Mwihaji na Nassoro Mashoto, Chuma alistaafu rasmi kucheza soka

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC