Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AKINA MKOJANI WAMETURUDISHIA LADHA ZA BONGO MUVI

Na Prince Hoza

BINAFSI mimi tangu walipoondoka kwenye tasnia ya maigizo hapa nchini nyota kama Steven Kanumba, Mzee Majuto, Sharo Milionea na Mzee Small niliona tasnia hiyo imeondokewa na watu muhimu sana. 

Kiwanda cha bongomuvi kama kinavyojulikana kwasasa nimekiona kama kimekaukiwa, wasanii waliobaki nimewaona kama wachanga na wameshindwa kuiweka kwenye matawi ya juu, nikianzia kwa Kanumba, yeye pekee aliisaidia bongomuvi kujitangaza nje ya mipaka yetu. 

Kanumba aliifanya Tanzania kujulikana na kuwafanya wasanii wetu kupiga hatua, wasanii wakubwa wa Nigeria haikuwa. 

Bongomuvi ilikosa ubunifu na ikajikuta kuwa kundi la umbea na kusemana vibaya wao kwa wao na kuleta tafrani, Kanumba alifariki dunia ingawa kazi zake bado ziliendelea kuitangaza Tanzania kimataifa, sawa na kazi za Mzee Majuto na Small Wangamba ambao nao walikuwa kivutio kwenye tasnia hiyo.


Wasanii hao waliaga dunia, bado mchango wao ni mkubwa sana, wakati mastaa hao wakifariki, kijana mwingine Sharo Milionea naye alikuja na aidia yake ambayo ilimtambulisha vilivyo, Sharo alikuwa muigizaji wa kwanza kukubalika na kuwavutia wawekezaji. 

Makampuni mbalimbali yalijitokeza kumdhamini na kuingia naye  mikataba, kifo chake kilisononesha wengi kwani ndio kwanza alichipukia kwenye sanaa hiyo.

Kufariki kwa Kanumba, Mzee Majuto, Sharo Milionea na Mzee Small kuliifanya bongomuvi kulemaa na wengi waliacha kutazama muvi za kibongo na kukimbilia muvi za nje. 

Hata mimi niliacha kabisa kununua muvi za nyumbani na kujikuta natazama muvi za Kihindi, Kikorea, Kijapan, Kituruki na kwingine, muvi hizo zinatafsiliwa na madj wetu wa kibongo kama Dj Murph, Dj Maki na wengineo. 

Chumvi Nyingi

Sio siri muvi za nje zinavutia, licha kwamba wasanii wa Tanzania walishindana kutoa muvi zao lakini walizidiwa ubunifu.

Malalamiko ya hapa na pale kuhusu wasanii wetu kutaka muvi za nje ziondolewe kwenye soko, lakini wengi waligoma wakidai kwamba muvi za Tanzania zimekosa ubunifu hivyo wengi walikimbilia huko.

Mimi binafsi niliwahi kuwaponda bongomuvi na nikawataka wawe wabunifu ili kazi zao ziweze kushindana na muvi na nje zinazotafsiliwa na madj wetu. 

Kadri siku zinavyozidi kusonga mbele na wasanii wetu wanabadilika na kuongeza maarifa, wasanii kama Mkojani, Tin White na Chumvi Nyingi ni miongoni mwa wasanii wanaoturudishia ladha za bongomuvi. 

Nimejaribu kutembelea maktaba {library} za kuuza muvi ambapo madj niliowakuta wamekiri kwamba muvi za bongomuvi zinakimbiza sokoni na haitachukua mda mrefu zitawafunika Wakorea, Wachina, Wahindi na Waturuki ambao sokoni waliongoza kwa mda wote. 

Mkojani

Chumvi Nyingi, Mkojani na Tin White ni moja kati ya wasanii walioifanya bongomuvi kufika hapo ilipo, tangu waondoke Kanumba, Mzee Majuto, Mzee Small na Sharo Milionea, akina Chumvi Nyingi wameturudishia ladha za bongomuvi. 

ALAMSIKI

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC