Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUWAACHA BALEKE NI PHIRI NI KUJIMALIZS AU KUJIJENGA UPYA?

Na Prince Hoza

KLABU ya Simba SC maarufu Wekundu wa Msimbazi imewaacha washambuliaji wake hatari Moses Phiri raia wa Zambia na Jean Baleke raia wa DR Congo, Simba imeamua kuwaacha washambuliaji hao baada ya kutoridhishwa na viwango vyao.

Mbali na kuwaacha washambuliaji hao, pia imewaacha na wachezaji wengine wazawa, klabu hiyo imeamua kufanya mabadiliko kwa kuwasajili wachezaji wapya wakiwemo washambuliaji na wa maeneo mengine.

Baada ya kutangaza kuwaacha washambuliaji hao, zimetoka lawama kutoka kwa baadhi ya mashabiki wake na wadau wa soka wakishangaa
kuwaacha Baleke na Phiri ingawa takwimu ziliwabeba. 

Nikianza kwa Phiri, takwimu zilimbeba mshambuliaji huyo aliyejiunga na Simba msimu uliopita akitokea Zanaco ya Zambia.

Mshambuliaji huyo alifanikiwa kufunga mabao 10 kwenye Ligi Kuu bara akiongoza kwa mabao kwenye timu yake na pia akishika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu bara akiwa nyuma ya Fiston Mayele aliyekuwa anaichezea Yanga SC. 

Hata hivyo Phiri aliumia katika ligi ikiwa inaendelea na kuumia kwake kulimuathiri katika ndoto zake za kuchukua kiatu cha dhahabu. 

Mwishoni mwa msimu Said Ntibanzokiza "Saido", John Bocco na Jean Baleke waliweza kuonyesha uwezo wao wa kufunga na kumpa changamoto Phiri.

Pia Mzambia huyo alikuwa msaada mkubwa Simba kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika akiiwezesha Simba kutinga hatua ya makundi huku yeye akiwa mmoja kati ya wafungaji wa timu. 

Hata msimu huu kwenye mechi za Ligi Kuu bara aliweza kupachika mabao matatu ingawa akucheza mechi nyingi. 

Kwa kifupi Simba imemuacha Phiri akiwa bado ana uwezo mkubwa wa kupachika mabao ingawa kwa mujibu wa kocha Abdelhak Benchikha anadai kwamba Phiri si lolote na timu yake inahitaji mshambuliaji hatari. 

Kwa upande wa Baleke, ambaye naye alijiunga na Simba kwa mkopo akitokea TP Mazembe ya DR Congo, alikuja kwenye dirisha dogo na aliweza kufunga mabao 9, moto wake wa mabao uliwatisha wengi na ikabidi apewe nafasi zaidi na msimu huu alikuwa tegemeo la timu. 

Mpaka Ligi Kuu bara inasimama kupisha kombe la Mapinduzi, Baleke alishapachika magoli 8 na assist moja katika mechi 9 alizocheza ni sawa na kuhusika na magoli kwenye mechi zote. 

Msimu uliopita Baleke alikuwa msaada mkubwa kwenye Ligi ya mabingwa Afrika katika hatua ya makundi, ambapo atakumbukwa kwenye mchezo wa Raja Casablanca na Wydad ambapo aliweza kupachika mabao. 

Sio siri Benchikha amependekeza Baleke na mwenzake Phiri waachwe akiamini kwamba hawana viwango vya kuipigania Simba. 

Binafsi mimi naona ni kama Simba inajimaliza yenyewe, lakini kwa upande wangu wa pili ni kama Simba inaenda kujijenga upya. 

Kabla ya ujio wa Benchikha, Simba ilikuwa inanolewa na Mbrazil Robert Oliviera "Robertinho" lakini kilio kikubwa cha Wanasimba ni kukosa matokeo mazuri na washambuliaji walionekana tatizo, ngoja tuone na tusubiri. 



ALAMSIKI

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC