Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BABACAR SARR ATABIRIWA MAKUBWA SIMBA


Kocha wa viungo wa timu ya Al Nassr ya Saudi Arabia, Junior Robertinho ambaye ni mtoto wa aliyekuwa kocha wa Simba, Robertinho Oliviera amesema kiungo mpya wa Msimbazi, Babacar Sarr ni mtu wa kazi

Sarr aliyesajiliwa msimu huu kutoka US Monastir tayari amecheza mechi mbili, kwani
aliposajiliwa tu alikuta timu ikiwania ubingwa wa Kombe la Mapinduzi Zanzibar.

Japokuwa Wekundu hao hawakutwaa kombe hilo mbele ya mabingwa watetezi Mlandege, Sarr ni miongoni mwa wachezaji
walioingia kipindi cha pili walipocheza dhidi ya Singida Fountain Gate, na fainali kocha
alimpanga kikosi cha kwanza ingawa inaonekana bado kuna mashabiki hawajamuelewa

Junior amesema amewahi kumuona kiungo huyo kwa muda wa dakika 90 walipocheza na US Monastir na alikuwa mchezaji hatari.

Alieleza kuwa, hakuna mchezaji ambaye hana matokeo kwenye timu halafu akachezeshwa mechi nzima na hiyo tu inaonyesha ni aina gani ya mchezaji Simba
wamempata.

"Niliwasikia makocha wake wakisema ni mchezaji mwenye nidhamu ya ukabaji na
tulipocheza nao alikuwa na utulivu mkubwa uwanjani na kupokonya mipira kwa haraka hasa kwenye kufungua njia za kupitisha mipira," alisema

Aliongeza kuwa kipaji chake kinaweza kuisaidia Simba ambayo alikuwa anaiona muda mrefu wakati baba yake alipoifundisha kuhitaji mtu mwenye uwezo wa kurudisha ugumu kwa timu pinzani uwasogelea mabeki wa kati.

"Baba yangu alikuwa ananiambia Tanzania soka lao linatumia nguvu Sana. Pengine hilo ndilo eneo ambalo Sarr anatakiwa ajipange nalo, kwani timu aliyotoka alikuwa ni kiungo mstaarabu hakUwa na matumizi makubwa ya nguvu"

Sarr anaonekana kuwa na kazi ya ziada ndani ya timu hiyo, kwani wachezaji anaocheza nao nafasi moja tayari walishaonyesha makali mbele ya kocha Abdelhak Benchikha na wanafahamiana namna ya uchezaji

Viungo anaocheza nao ni Mzamiru Yasin, Fabrice Ngoma, Sadio Kanoute na Abdallah
Hamisi

Babacar Sarr atabiriwa makubwa Simba

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC