Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA IMEPAMBANA ILA BAHATI HAIKUWA YAO

BAHATI haikuwa yao Wekundu wa Msimbazi, Simba SC dhidi ya Al Ahly Jumanne iliyopita mchezo wa marudiano uliofanyika jijini Cairo. 

Katika mchezo huo wa michuano ya African Football League, timu hizo zilifungana mabao 1-1 na kufanya ziwe zimefungana kwa jumla ya mabao 3-3, katika mchezo wa kwanza uliofanyika jijini Dar es Salaam katika uwanja wa Mkapa timu hizo zenye ushindani wa aina yake zilitoka sare ya kufungana mabao 2-2. 

Sare ya jijini Dar es Salaam iliwafanya Simba kuaga michuano hiyo licha kwamba zilitoka sare tena jijini Cairo, magoli mawili ya ugenini yaliipa faida Ahly na kusonga mbele. 
Al Ahly sasa itakutana na Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini hatua ya nusu fainali, Ahly ndio mabingwa wa kihistoria wa Afrika.

Na pia ni mabingwa watetesi wa Ligi ya mabingwa Afrika, uwezo mkubwa ilionao sidhani kama timu nyingine inayoweza kukabiliana nayo kwani imekuwa ikizitesa timu inazokutana nazo. 

Ingawa imekuwa ikikutana na upinzani mkali hasa na timu nyingine za kiarabu kutoka Afrika kaskazini na hivi karibuni ilifungwa bao 1-0 na timu ya USM Alger ya Algeria. 

Katika mchezo huo wa kuwania ubingwa wa Super Cup, ambao ulishirikisha mabingwa wa Ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho, zaidi ya hapo Ahly imekuwa kiboko yao na ikiendelea kuogopwa. 

Simba SC nayo ilikuwa miongoni mwa timu iliyopangiwa kukutana na Al Ahly, mashabiki wa Simba waliingiwa mchecheto walipopangiwa kucheza na Al Ahly, wakati ratiba ya michuano hiyo inapangwa na Ahly mashabiki wengi wa soka nchini waliikatia tamaa Simba. 

Ukiondoa TP Mazembe ya DR Congo ambayo ilikuwa ikiipa ushindani mkubwa, lakini sasa TP Mazembe imepungua makali yake, lakini Simba ni timu pekee Afrika mashariki kuweza kukabilia vikali na Ahly. 

Ushindani wa Simba haukuanzia katika mchezo wa kombe la African Football League, Wekundu hao wa Msimbazi walianza kuchuana vikali na Ahly kuanzia miaka ya 1985 ambapo Simba iliweza kuifunga mabao 2-1 katika uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza, wakati huo michuano hiyo ikijulikana kama Klabu bingwa Afrika. 

Lakini tena zilikutana msimu wa mwaka 2018/2019 zikicheza uwanja wa Mkapa mjini Dar es Salaam na Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0, pia zilikutana tena msimu wa 2020/2021 katika uwanja huo huo wa Mkapa na Simba kushinda bao 1-0. 

Tofauti na mechi iliyopita ambayo ilikuwa ya mtoano ya michuano mipya ya African Football League, wengi walidhani Simba itapigwa magoli mengi hasa kutokana na Ahly kupania mchezo huo.

Na pia imefanya usajili kabambe ambapo miongoni mwa wachezaji bora waliosajiliwa ametoka barani ulaya kwenye timu ya Dortmund ya Ujerumani. 

Hata hivyo Simba walicheza kandanda safi na iliwafanya Ahly kumtimu kocha wake, kwani Wekundu hao waliupiga mwingi na kama si bahati kwa Ahly wangefungwa nyumbani na kutolewa kwenye mashindano, kwani Ahly walisawazisha baada ya kufungwa. 

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC