Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTANZANIA KUWANIA UBINGWA WA WBC UTURUKI

Bondia Pius Mpenda a.k.a 'Super Hero' kutoka Naccoz gym chini ya kocha wake Rama Jah tarehe 29/10/2023 anatarajiwa kupanda ulingoni kwenye pambano la kimataifa nchini Uturuki.

Wastani wa Mpenda kwenye mapambano yake ya kimataifa nnje ya mipaka ya Tanzania umekuwa mzuri amecheza jumla ya mapambano matatu ya kimataifa ameshinda mawili na kupoteza moja na amefanikiwa kutwaa mkanda mmoja wa dunia wa WBU.

Mpenda atacheza na bondia Dauren Yeleussinov mzaliwa wa jiji la Kayindy nchini Kazakhstan ila ni mkazi wa jiji la Brooklyn, New York nchini Marekani.

Mpenda na Yeleussinov watacheza pambano la raundi 10 ubingwa wa WBC (World Boxing Council Peace Super Welterweight kg 69 title) litakalo fanyika kwenye ukumbi wa Hilton Double jijini Instanbul nchini Uturuki.

Mpinzani wake Mpenda bondia Yeleussinov alianza safari yake ya mchezo wa masumbwii kupitia ngumi za Amateur (Ngumi za Ridhaa) tarehe 17/12/2005 dhidi ya bondia Ruslan Safiullin raia wa Kazakhstan kwenye pambano la raundi 4 na bondia Yeleussinov aliweza kushinda pambano hilo kwa matokeo ya point .

Mpaka anatoka kwenye ngumi za Amateur alikuwa na rekodi yakucheza jumla ya mapambano 37, kashinda 26, kwa "KO'S" 1, kapoteza 11 na sare 0.

Aliingia kwenye ngumi za Kulipwa (Professional Boxing) tarehe 3/12/2014 dhidi ya bondia Anthony Dwayne raia wa Marekani kwenye pambano la raundi 4 na bondia Yeleussinov aliweza kushinda pambano hilo kwa matokeo ya "TKO" kwenye raundi ya kwanza.

Mpaka sasa ni bondia mwenye hadhii ya nyota moja anacheza kwenye uzani wa Super Welterweight Kg 69 anashikilia nafasi ya 342 kati ya mabondia 1898 Duniani na nafasi namba 2 kati ya mabondia wa 5 wanaocheza uzito huo wa kg 69 nchini kwao Kazakhstan.

Akiwa na rekodi yakucheza jumla ya mapambano 14, Kashinda 11, Kwa "KO'S" 10, kapoteza 2 na sare 1.

Mpenda ni bondia mwenye hadhii ya nyota mbili anacheza kwenye uzani Middleweight kg 72 anashikilia nafasi ya 114 kati ya mabondia 1551 Duniani na nafasi namba 1 kati ya mabondia 28 wanaocheza uzito huo wa kg 72 hapa nyumbani Tanzania.

Akiwa na rekodi yakucheza jumla ya mapambano 8, kashinda 7, kwa "KO'S" 4, kapoteza 1 na sare 0.
Tunamtakia maandalizi mema bondia Pius Mpenda iliaweze kuipeperusha bendera ya Tanzania vyema.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC