Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MJUE IDDI NADO: KUTOKA MBEYA CITY HADI AZAM FC

Na Abdul Makambo

Wakati anatoka Mbeya City Kujiunga na Azam fc alikua kwenye kiwango bora sana

Alifanya Vyema alianza kuwatumia matajir hao wa Chamazi na Alikuwa mmoja wa Mawinga bora nchini

Klabu nyingi zilimtamani na timu ya Taifa ikawa ni Uwanja wake wa Nyumbani kutokana na kiwango chake bora sana

Ni moja ya Mawinga wa Kisasa ambao sifa zao sio Mbio tu bali Ubunifu,uwezo wa kuwatoka mabeki wakiwa wanalitafta lango

Iddy Nado ni mmoja wa Mawinga Wachache ambao uwezo wao ni mkubwa sana.

Kasi
Ufundi
Kufunga mabao

Bahati Mbaya alikuja akapata Majeraha yakamuweka nje karbia msimu mmoja kama sio miwili

Mwaka Jana akaanza taratibu kurejea kwenye kikosi lakin kama unavyojua majeraha ya Goti sio rahisi kurejea kwa kasi

Akaanza kupewa muda lakin bado hakuonekana Nado kila mtu anayemjua lakin ndo kwanza alikua amerejea hivyo alihtaji mda kuwa sawa

Kuisha kwa Ligi na Kwenda kujiandaa Kwa ajili ya msimu huu ni karata aliyoitumia vyema kurejea kwenye ubora wake...

Msimu huu Tangu alipoanza kuaminiwa Tumeanza kumuaona Iddy Nado wa Wa Mbeya City,Nado wa Azam fc msimu wa kwanza akiwa ametoka Mbeya City....

Ni Dhahiri Gari la Iddy Limewaka sana na Binafsi mie ni shabiki wake sana tangu akiwa Mbeya Ule mwendo wake na uwezo wa Kuwatoka Mabeki ndo Vitu Nilivutiwa navyo 👏👏👏

This Time round Karudi vyema Na Mungu Amsaidie Aepukane na Majeraha Ili Tufurahia kipaji chake bora sana..

Taratibu ameanza kujikatia kipande chake ndani ya kikosi cha kwanza cha Azam fc na akiendelea hivi hakuna wa kumuweka Nje..👇

Anatengeneza magoli kwa wenzie
Anafunga pale inapobidi
Sio Kipenzi cha Mabeki wasio na kasi
Ukitaka Mwendo na Ufundi atakupa tena zaidi na zaidi.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC