Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA POWER DYNAMOS AIGWAYA SIMBA

Baada ya kutinga Raundi ya Kwanza ya mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuing’oa African Stars ya Namibia kwa faida ya bao la ugenini na kutambua sasa itavaana na Simba SC, Kocha Mkuu wa Power Dynamos ya Zambia, Mwenya Chipepo ameonekana kuingiwa ubaridi akisema anawafahamu vizuri wapinzani wao ili na sasa wanajipanga upya kuvunja rekodi ya Wekundu hao.

Dynamos imetinga hatua hiyo baada ya awali kufungwa 2-1 ugenini kisha jumamozi (Agosti 26) ikalipa kisasi nyumbani kwa kushinda 1-0 na kufanya matokeo ya mwisho kuwa 2-2 na kupenya kwa kanuni ya faida ya bao la ugenini na itavaana na Simba SC mwezi ujao ikiwa ni mwezi mmoja tangu zikutane kwenye pambano la kirafiki la kimataifa kwenye Tamasha la Simba Day na miamba hiyo ya Zambia kulala 2-0 Kwa Mkapa.

Akizungumza kutoka nchini Zambia, Chipepo alisema sio wageni kwa Simba SC, wanaifahamu vizuri kuanzia ubora wao wa timu na rekodi zao kwenye michuano hiyo, hivyo wanajipanga ili kuivunja, kwani kwa miaka ya hivi karibuni, Simba SC imekuwa ikifuzu makundi na kukwamia Robo Fainali ya Michuano ya CAF.

Simba SC ni timu nzuri na ina wachezaji wengi wenye zoefu, tumecheza nao mechi ya kirafiki Agosti 6 mwaka huu tukafungwa mabao 2-0, kilikuwa ni kipimo sahihi kwetu tumesawazisha makosa na kufanikiwa kutinga hatua ya kwanza,” amesema Chipepo na kuongeza

“Kukutana nao sio habari mpya kwetu tulitarajia kitu hiki tutaingia kwa kuwaheshinu kutokana na rekodi yao nzuri dhidi yetu na ubora wao kwenye michuano hii, malengo yetu ni kutinga hatua ya makundi tutapambana kuhakikisha lengo hilo linatimia.”

Chipepo amesema wanafahamu ubora wa kikosi cha Simba SC ulipo na udhaifu wao hivyo watapambana kuhakikisha wanafanya jitihadi za kuwadhibiti ili waweze kuweka heshima katika mechi za mashindano.#

Akizungumzia ubora wa mchezaji mmoja mmoja ndani ya kikosi cha Simba SC amesema kila mchezaji aliye ndani ya kikosi cha timu hiyo ni bora na ndio maana kasajiliwa, hivyo hawezi kuzungumzia mchezaji mmoja mmoja.

“Naheshimu kila mchezaji na wachezaji wangu mara baada ya kutinga hatua inayofuata tulikaa pamoja na kukumbushana aina ya timu tunayoenda kukutana nayo.”


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC