Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mjue Gift Fred, beki mpya wa kati aliyechukua nafasi ya Mamadou Doumbia

Na Salum Fikiri Jr

MIAKA kadhaa iliyopita Yanga SC lilikuwa jina kubwa nchini Uganda hasa kwa sababu ilizoeleka mara kwa mara kwenda kucheza na timu za huko na pia kusajili wachezaji mbalimbali. 

Ikumbukwe mwaka 1993 na 1999 Yanga ilienda kushinda ubingwa wa Klabu biogwa Afrika mashariki na kati, maarufu kombe la Kagame, Yanga iliweza kusajili nyota mbalimbali nchini Uganda kama Hamisi Kiiza "Diego" ambao walitokea kujipatia umaarufu mkubwa. 

Yanga ikapotea machoni mwa Uganda na likabaki jina tu ambalo linaendelea kusikika pande mbalimbali za Afrika na dunia, umaarufu wa Yanga unatokana na na uwezo wake uliouonyesha msimu uliopita ambapo iliweza kufika fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika, pia iliweza kushinda ubingwa wa Ligi Kuu bara na mengineyo. 

Ingawa tayari ina mchezaji kutoka Uganda Khalid Aucho, ikitaka kujiimarisha zaidi ili kushindana ndani na nje ya nchi. Kikubwa wanachokiangalia Yanga ni kufika makundi Ligi ya mabingwa barani Afrika.

Baada ya msimu uliopita kumsajili beki wa kati Mamadou Doumbia raia wa Mali, bado Yanga haijafanikiwa kwani mchezaji huyo alishindwa kupata namba kwenye kikosi cha kwanza.

Doumbia alisajiliwa kwa lengo la kusimama katikati akicheza na Bakari Mwamnyeto au Dickson Job, kushindwa kwake Doumbia kulimfanya kocha Nasreddine Nabi raia wa Tunisia kumtumia Ibrahim Baka kama sentahafu. 

Baada ya kumalizika msimu wa 2022/2023 huku Yanga ikishinda mataji yote matatu, ikiwemo kombe la Azam Sports Federation Cup, ASFC au kombe la FA. 

Na pia ilianza na kubeba Ngao ya Jamii mwanzoni mwa msimu, dirisha kubwa la usajili limefunguliwa na Yanga ikaamua kuanza na beki wa kimataifa kutoka nchini Uganda. 

Sio siri mabingwa hao wa Tanzania bara walianza kumfuatilia kwa kina Gift Fred anayeichezea timu ya SC Villa inayoshiriki Ligi Kuu ya Uganda, pia timu ya taifa, The Cranes. 

Gift ni beki wa kati anayecheza namba 5 au 4 na ana uwezo mkubwa wa kunyang' anya mipira, Gift ana ball control ni beki wa kisasa anajua kupiga pasi, anapiga chenga za maudhi anapanda mbele na kufunga.

Gift anaokoa kwa kuruka vichwa anacheza takolini, ana nguvu na anajua kukaba, kwa kifupi Yanga imepata beki mpambanaji na ndio maana The Cranes wamemfanya awe nahodha msaidizi. 

Beki huyo alionekana kwa mara ya kwanza dhidi ya Kaizer Chief katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam ambapo Yanga ilishinda bao 1-0. 

Mchezo huo ulikuwa wa maadhimisho ya Wiki ya Wananchi, Gift alizaliwa 1998  



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC