Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SPIDER AWAJIBU WANAOMTUHUMU KUDHULUMU HAKI ZA MAMBO POA

Na Fazila Lyimo

Hatimaye memba wa lililokuwa kundi la muziki wa kizazi kipya la Mambo Poa, Rashid Mustapha "Spider" amewajibu baadhi ya mashabiki wa kundi hilo kwamba yeye ahusiki na haki za waliokuwa wanamuziki wenzake wa kundi hilo ambao sasa ni marehemu. 

Akizungumza na chombo kimoja cha habari kupitia kipindi chake kinachorushwa mchana, alisema yeye asimamii kazi za wasanii hao wenzake ambao kwa sasa wametangulia mbele yaki. 

Spider aliwataja wenzake hao John Mjema na Steve 2k ambao wameaga dunia lakini walifanikiwa kuachia nyimbo mbalimbali ambazo zilitikisa.

Spider amedai kwamba kwa bahati mbaya kazi zao hazijawekwa kwenye mitandao hivyo ni ngumu yeye kuzisimamia, hata hivyo Spider amedai kuwa John Mjema na Steve 2k kila mmoja anawakilishwa na ndugu zake hivyo itakuwa ngumu kwa yeye kusimamia kazi zao. 

Hivi karibuni baadhi ya mashabiki wa kundi hilo walimjia juu Spider wakidai kwamba anahusika kutafuna mapato ya Steve 2k na Mjema kwakuwa wenzake hao hawapo duniani, jambo ambalo Spider ameweka wazi kwamba yeye ahusiki kabisa. 

Kundi la Mambo Poa lililokuwa na nyota hao watatu lilifanikiwa kupata umaarufu nchini kutokana na wimbo wake uitwao 'Mimi sio mwizi' na nyingine Spea tairi.

 
 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...