Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Makala: NI DHARAU KUBWA KUMLINGANISHA NA KAGERE

NIMETEMBELEA baadhi ya kurasa za mitandao ya kijamii hasa kwenye Facebook, Instagram na magroup ya Whatsaap ambapo baadhi ya wadau wakafikia hatua ya kuwafananisha Fiston Kalala Mayele na Meddie Kagere. 

Kilichonishangaza na kuona ni dharau kubwa waliyomfanyia mshambuliaji wa kimataifa wa DR Congo Fiston Mayele ambaye pia ni mshambuliaji tegemeo wa Yanga SC, kumfananisha Mayele na Kagere ni dharau. 

Watu walioleta ushindani huo wa Mayele na Kagere ulitokana na Kagere wa misimu minne iliyopita na Mayele wa sasa, ushindani huo wa Mayele sio na Kagere wa sasa anayeichezea Singida Big Stars kwa mheshimiwa Mwigulu Nchemba. 

Na pia simdharau Kagere, kwani ni mmoja kati ya washambuliaji hatari waliowahi kung' ara kwenye Ligi Kuu bara na kuweza kuibuka mfungaji bora misimu miwili mfululizo.

Kagere alisajiliwa na Simba msimu wa 2018/2019 akitokea Gor Mahia ya Kenya na alifanikiwa kuibuka mfungaji bora ndani ya msimu wake wa kwanza. 

Mshambuliaji huyo wa kati alivunja rekodi za Amissi Tambwe na Emmanuel Okwi ambao kila mmoja alifunga magoli 21, Kagere msimu wake wa kwanza mbali ya kuiwezesha Simba kutetea ubingwa wa bara, alifanikiwa kufunga magoli 23.

Uganda, hakuweza kufunga zaidi ya bao moja, isipokuwa Simba ilimtegemea sana Clatous Chama kwenye ufungaji na si yeye. 

Na hiyo ndio tofauti ya Kagere na Mayele, ambaye alisajiliwa na Yanga msimu uliopita akitokea timu ya AS Vita Club ya DR Congo.



Msimu wake wa kwanza Mayele alifunga mabao 16 na kushika nafasi ya pili, nyuma ya George Mpole wa Geita Gold aliyefunga magoli 17 na kuibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu bara. Ingawa alikuwa mfungaji namba mbili.

Mayele alitokea kukubalika sana na mashabiki wa soka nchini, iwe mkubwa, kijana na mtoto wote walimkubali sana Mayele.

Achana na staili yake ya ushangiliaji, Mayele ni mshambuliaji hatari kumzidi Kagere. 

Msimu huu Mayele ndie kinara wa mabao Ligi Kuu bara, kwani mpaka sasa ana mabao 16 na anayemfuatia ana mabao 10 huku ligi zikibakia mechi mbili na tayari Yanga imeshatwaa mara mbili mfululizo. 

Umahiri wa Mayele haujaishia kwenye ligi ya bara peke yake kama ilivyo kwa Kagere, Mayele amehamishia makali yake kimataifa na tayari ameisaidia Yanga kuingia fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. 

Haijaishia hapo, Mayele ni kinara wa mabao wa michuano hiyo ambapo mpaka sasa amefunga magoli 6. 

Ni dhambi kumlinganisha Mayele na Kagere. 
Asanteni





Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC