Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Makala; Yanga imeweka historia Afrika

NA ABDUL MAKAMBO
Call. 0787905328. 

TAREHE 19-3-2023 siku ya Jumapili, tarehe na mwaka wa kihistoria kwa klabu ya Dar Young Africans au Yanga iliifunga wawakilishi wa Tunisia us Monastir magoli 2-0 kwenye uwanja wa Mkapa jijini.

Kwa hakika Yanga imeleta furaha kubwa kwa wanachama, wapenzi na heshima kubwa kwa taifa la Tanzania.

Ni baada ya miaka mingi-Yanga iliingia robo fainali kwa mara ya kwanza na ilikuwa ni michuano ya Klabu bingwa barani Afrika mwaka 1969 kule Addis Ababa kule nchini Ethiopia na Yanga ikatolewa kwa shilingi.



2.Tokea mwaka ule yanga haikufanya tena vizuri na mwaka 1998 yanga ndipo ilipofanikiwa kuingia kwenye hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani afrika-ilicheza na apr ya rwanda ikaitoa na ikacheza na coffe ya ethiopia na ikaitoa na yanga ikaingia hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani afrika.Na kwenye makundi ilikua kundi moja na raja casablanca ya moroco.

Asec Mimosas ya Ivory Coast na Maning Rangers ya Afrika Kusini na Yanga ilikuwa chini ya kocha Tito Mwaluvanda na akaletwa Raoul Shungu raia wa DRC.

Na Yanga ilipata bahati nyingine tena mwaka 2016 Yanga ikiwa chini ya mfadhili Yusufu Mehboub Manji na kocha Mholanzi Hans Pluijm.

Na ilicheza Klabu bingwa na Gelgada Esperanca ya Angola na ilicheza na Al Ahry ya Misri.

Na Yanga iliangukia kwenye michuano ya Shirikisho Afrika.Ikicheza na Medeama ya Ghana, Mo Boejaia ya Algeria na Rayon ya Rwanda.

Natoka miaka hiyo Yanga haijafanya vizuri kwenye Klabu bingwa na hata kombe la Shirikisho.

Lakini ujio wa kocha Mtunisia Nasreddin Mohamed Nabi umekuwa ni mwanzo mzuri na bora kwa klabu ya Yanga na uwepo wa ufadhili GSM ni moja ya neema kwa klabu ya Yanga.

Nabi ni kocha mwenye falsafa  nzuri, kwa mafanikio  ya Yanga kuingia robo fainali ya Shirikisho Afrika italeta maendeleo na mafanikio makubwa ndani ya klabu ya Yanga.

Nabi leo ameweza kuwainua viwango akina Feisal Sakum au Feitoto, Fiston Mayele, Djuma Shaban, Joyce Lomalisa Mutambala, Farid Mussa na Clement Francis Mzize.



Kwa kweli wamepanda na wamebadilika kisoka na yote ni maelekezo na falsafa ya kimbinu ya kocha Nabi.

Kwa hakika Yanga imefanya makubwa na kocha Nabi atawapeleka mbali itachanua zaidi kwenye mashindano ya kimataifa.pongezi ziwaendee mlinda mlango Djigui Diarra Yanick Bangala, Khalid Aucho, Stephano Aziz Ki na Kennedy Musonda na wengineo.
Asanteni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC