Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wanachama Simba sasa wakataa 'Mbumbumbu' kuwania Urais, Ujumbe

Na Saida Salum. Dar es Salaam

Mkutano mkuu wa wanachama uliofanyika hii leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Ocean Road ulioudhuriwa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dr Harrison Mwakyembe umepitisha katiba mpya ya kuelekea kwenye kampuni ambapo sasa Simba itaendeshwa kwa Hisa.

Katika mkutano huo ulioitishwa na kaimu Rais wa klabu hiyo, Salim Abdallah "Try Again", na kuudhuriwa na zaidi ya wanachama 1000 ulipitisha mpango wa kuuza Hisa asilimia 49 kwa mwekezaji na asilimia 51 kubaki kwa wanachama kama ambavyo serikali imezitaka klabu za wanachama kufanya hivyo.

Tayari mfanyabiashara, Mohamed 'Mo' Dewji ambaye alikuwa mwanachama pekee wa klabu hiyo kujitokeza na kutaka kununua Hisa asilimia 51 kwa kumwaga Bilioni 20 alisharidhia kununua Hisa asilimia 49 hivyo leo ilikuwa kazi ndogo tu kurekebisha baadhi ya vifungu.

Wanachama haowalikubaliana Simba ijiendeshe kisasa na huenda msimu ujao ikatumia uwanja wake wenyewe kuchezea mechi zake za Ligi Kuu Bara na mechi za kirafiki, pia wanachama wameamua kuwa hawataki tena mbumbumbu kuwania vyeo vya ngazi ya juu kwani kuanzia Rais (Mwenyekiti wa Bodi) na wajumbe wake wanne wawe na shahada.

Pia nafasi ya katibu mkuu nayo imefutwa rasmi na sasa kutakuwa na mkurugenzi mtendaji ambaye atawajibika kama katibu, aidha mwanamke mmoja atachaguliwa kuwa mjumbe ili kuweka uwiano sawa

Wanachama wa klabu Simba walikutana leo kujadili mambo yao

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC