Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Pazia la Ligi Kuu Bara kufungwa leo

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/18 linafungwa leo kwa mechi nane kupigwa katika viwanja mbalimbali hapa nchini, ligi hiyo inafikia tamati ikiwa bingwa ameshapatikana ambaye ni Simba SC.

Vita pekee iliyosalia ni ya kumsaka mshindi wa pili ambayo inawaniwa vikali na timu za Azam Fc na Yanga Sc ambao leo wanaumana usiku katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo Azam wana pointi 55 na Yanga ina pointi 52 hivyo nafasi iko wazi kwa Yanga endapo itashinda ila Azam inahitaji sare.

Pia vita ipo kwa timu mbili za Ndanda Fc ya Mtwara na Majimaji Songea ambapo moja leo itaungana na Njombe Mji kushuka daraja.

Ratiba kamili hii hapa

Yanga Sc vs Azam Fc Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuanzia saa 2;00 usiku.

Majimaji Fc vs Simba SC uwanja wa Majimaji Stadium mjini Songea.

Kagera Sugar vs Lipuli Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Tanzania Prisons vs Singida United Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Ndanda Fc vs Stand United Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mtibwa Sugar vs Mbeya City Uwanja wa Manungu Complex mjini Morogoro.

Mbao Fc vs Ruvu Shooting Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Njombe Mji vs Mwadui Fc Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe na hii itakuwa mechi ya mwisho ya Ligi Kuu kuchezwa mjini Njombe

Ligi Kuu Bara inamalizika leo kwa timu zote 16 kushuka uwanjani

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC