Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Nyota watano waliokatia umeme Simba mbele ya Rais Magufuli

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Mabingwa wa soka nchini Simba SC walipokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Simba ilipokea kichapo hicho mbele ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli siku ya Jumamosi ya Mei 19 mwaka huu, Simba ilikabidhiwa ubingwa wake ilioutwaa Mei 10 mwaka huu na hasa baada ya mahasimu wao Yanga kulala mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Katika mchezo kati ya Simba na Kagera ulioudhuriwa na Rais Magufuli, Simba ilijikuta ikibanwa na kuchapwa bao hilo moja lililofungwa na Christopher Edward ambaye alilelewa na Simba.

Wafuatao ni nyota wanne ambao waliikatia umeme Simba SC mbele ya Rais Magufuli

1. Juma Kaseja

Kipa mkongwe aliyepata kuzichezea Simba na Yanga kwa nyakati tofauti, kipa huyo alikuwa kikwazo kwa washambuliaji wa Simba ambao walishindwa kumfunga, sifa yake kubwa kwenye mchezo huo ni pale alipoweza kuokoa penalti iliyopigwa na Emmanuel Okwi.

2. Juma Nyoso

Naye amewahi kuichezea Simba pamoja na Coastal Union, alikuwa kizingiti kikubwa na kuweza kuwadhibiti washambuliaji hatari wa Simba ambao wanasifika kwa kucheka na nyavu, Nyoso alifanya kazi kubwa ya kuzuia mashambulizi yote ya Simba.

3. George Kavila

Kiungo huyu mkongwe aliingia kipindi cha pili lakini alionyesha kuwadhibiti Simba na kufanya matokeo ya mchezo kuwa hivyo, Kavila hakuwa na masihara mbele ya Rais Magufuli kwani kila mpira aliouona mbele yake aliuondosha.

4. Christopher Edward

Mfungaji wa goli pekee la ushindi lililomsababishia Rais Magufuli apeleke sifa kwa Kagera Sugar badala ya Simba ambao ndio mabingwa wa soka nchini, Edward alifunga bao la ushindi.

5. Peter Mwalyanzi

Naweza kusema huyu ndiye mkata umeme kwa viungo wa Simba ambao haakufua dafu kwake mpaka Rais Magufuli akatamka maneno kuwa kwa Simba hii kimataifa bado, Mwalyanzi aliwahi kuichezea Simba akitokea Mbeya City ya jijini Mbeya

Juma Kaseja aliikatia umeme Simba

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC