Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ngasa kurejea Yanga kwa mara ya tatu

Na Saida Salum. Dar es Salaam

Klabu ya Yanga iko mbioni kumalizana na kiungo mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngasa wa Ndanda Fc ya Mtwara kwa mkataba wa mwaka mmoja imebainika, taarifa zilizosambaa jana zinasema tayari mchezaji huyo ameshazungumza na viongozi wa klabu hiyo na muda wowote kuanzia sasa anaweza kumwaga wino.

Ngasa amecheza vizuri akiwa na Ndanda Fc na kuipigania timu hiyo kusalia Ligi Kuu Bara mpaka mabosi wa Yanga kuvutiwa naye na kuamua kumrejesha tena mitaa ya Jangwani kwa mara ya tatu, Ngasa alijiunga Yanga kwa mara ya kwanza mwaka 2006 akitokea Kagera Sugar ya Bukoba kabla hajanunuliwa na Azam Fc kwa usajili uliovunja rekodi mwaka 2010, nyota huyo akidumu Azam Fc na baadaye akajiunga na Simba kabla hajarejea Yanga kwa mara pili.

Ngasa hakudumu sana Jangwani kwani akajiunga na Free State Stars ya Afrika Kusini ambako nako hakudumu akavunja mkataba na kujiunga na Fanja ya Oman, pia hakudumu akarejea nyumbani Tanzania na kujiunga na Mbeya City aliyodumu nayo kwa nusu msimu kabla hajajiunga na Ndanda Fc, Akiwa na Ndanda, Ngasa ameonyesha kiwango kizuri ambapo Yanga kwa mara ya tatu wanaamua kumrejesha tena kikosini, mchezaji huyo juzi alionekana mitaa ya klabu hiyo Jangwani akisalimiana na wapenzi na mashabiki wa klabu hiyo.

Jana uongozi wa Yanga ulipinga vikali usajili wa Ngasa na ikidai mchezaji huyo alienda Jangwani kuwasalimia tu na hawana mpango wa kumrejesha, lakini taarifa mpya zinasema Ngasa ni miongoni mwa wachezaji wapya wa Yanga watakaoshiriki katika mashindano yajayo ikiwemo kombe la Shirikisho barani Afrika

Mbali na Ngasa, Yanga pia inatajwa kutaka kumsainisha mshambuliaji wa Simba Mohamed Ibrahim "Mo" na kiungo wa Mbao Fc ya Mwanza, Habib Kiyombo

Mrishp Ngasa kurejea tena Yanga

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...