Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: Kichuya kuvunja rekodi ya Omari Hussein Keegan?

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Rekodi ya mfungaji wa magoli matatu (Hat trick) inashikiliwa na King Abdallah Kibaden Mputa wa Simba Sc ambaye alifunga mabao hayo mwaka 1977 wakati Simba ilipoibugiza Yanga mabao 6-0 uwanja wa  Taifa Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu bara.

Lakini mshambuliaji wa Yanga Sc, Omari Hussein wengi walimpachika jina la utani Keegan wakimdananisha na mwanasoka wa kimataifa ulimwenguni, Kevin Keegan, Omari Hussein ni mchezaji wa Yanga yeye ameweka rekodi ya kuwa mfungaji wa muda wote wa mechi za watani Simba na Yanga.

Keegan amefunga jumla ya magoli sita ambayo ni mengi na mchezaji pekee anayekaribia kumfikia ama kuweza kuivunja rekodi hiyo ni kiungo mshambuliaji wa Simba Sc, Shiza Kichuya ambaye yeye amefunga mabao manne mpaka sasa.

Keegan alianza kufunga tangu Septemba 18, 1982 Yanga ilipoifunga Simba mabao 3-0, Keegan alifunga mabao mawili dakika ya 2 na 85 huku goli lingine likifungwa na Makumbi Juma dakika ya 62.

Keegan alifunga tena Aprili 16, 1983 Yanga ikiichapa tena Simba mabao 3-1, wafungaji wa Yanga walikuwa Charles Mkwasa dakika ya 21, Makumbi Juma dakika ya 38 na Keegan dakika ya 84 goli pekee la Simba lilifungwa na Musa Kihwelo dakika ya 14.

Machi 10, 1984 Yanga na Simba zilitoka sare ya kufungana bao 1-1, Omari Hussein Keegan akaifungia Yanga bao dakika ua 72 wakati bao la Simba lilifungwa na kipa Idd Pazi kwa mkwaju wa penalti dakika ya 20.

Mei 19, 1985 Yanga na Simba zilitoka tena sare ya kufungana bao 1-1 na Omari Hussein Keegan akaifungia Yanga bao dakika ya 6 na Simba wakapata bao kupitia Mohamed Bob Chopa dakika ya 30.

Agosti 23, 1986 safari hii Simba ikaifunga Yanga mabao 2-1 yaliyofungwa na Edward Chumila dakika ya 9 na Malota Soma dakika ya 51 wakati goli pekee la Yanga lilifungwa na Keegan dakika ya 5, jumla mshambuliaji huyo Omary Hussein Keegan anaweka historia ya kuwa mfungaji wa wakati wote wa mechi za watani wa jadi Simba na Yanga

Miamba hiyo inaumana siku ya Jumapili katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam

Shiza Kichuya anakaribia kuvunja rekodi ya Omary Hussein Keegan wa Yanga

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC