Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUELEKEA SIMBA NA YANGA JUMAPILI, REKODI YA KIBADEN YAWAUMIZA VICHWA OKWI, BOCCO NA CHIRWA

Na Paskal Beatus. Dar es Salaam

Mwaka 1977 Simba Sc almaarufu Wekundu wa Msimbazi au wana Lunyasi waliinyanyasa Yanga Sc kwa kuichapa mabao 6-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara uwanja wa Taifa (Sasa Uhuru Stadium).

Mshambuliaji wa Simba wakati huo Abdallah Seif Athuman Kibaden aliifungia Simba mabao matatu katika mchezo huo huku mengine mawili yakifungwa na Jumanne Khamis Masimenti na goli lingine Yanga walijifunga.

Basi mpaka sasa imepita takribani miaka 39 hakuna mchezaji yeyote si wa Simba wala Yanga aliyeweza kumfikia Kibaden kwa kufunga mabao matatu kwenye mchezo mmoja wa watani.

Lakini Jumapili ijayo watani hao wa jadi wa soka la Tanzania wanaumana katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, Simba wao wana washambuliaji watatu ambao wanaweza kufanya lolote katika mchezo huo kwa kuvunja rekodi ya Kibaden.

Simba wanaye Emmanuel Anord Okwi, John Raphael Bocco na Shiza Kichuya ambao wanaweza kumfikia Kibaden ingawa wafanye kazi kwelikweli kuupita ukuta wa Yanga ulio chini ya Kevin Yondan na Abdallah Shaibu "Ninja" au Andrew Vicent "Dante", na Yanga wanao watu hatari kama Obrey Chirwa, Raphael Daudi au Pius Buswita ambao kila mmoja anaweza kuvunja rekodi ya Kibaden.

Ukuta wa Simba una watu mahiri kama Salim Mbonde, Jjuko Murushid au Yusuph Mlipili ambapo unaweza usiamini kuwa huenda Kibaden akaendelea kutesa na rekodi yake ya Hat trick ndani ya Simba na Yanga "Derby"

Abdallah Kibaden (Pichani) rekodi yake huenda ikavunjwa Jumapili

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC