Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KISPOTI

SIMBA KUMTOA MO IBRAHIM KWA MKOPO NI JAMBO LA BUSARA SANA

Na Prince Hoza

SIMBA SC na Yanga Sc zinaumana Jumapili ijayo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, hiyo ni mechi kubwa hapa nchini ambapo wapenda soka watajitokeza kushuhudia mtanange huo.

Lakini jina la Mo Ibrahim halimo katika kurasa za magazeti ya michezo hasa ya hapa nchini, Mo Ibrahim ni mchezaji wa Simba Sc ambao kwa sasa wanaongoza ligi, Simba wapo kileleni kwa pointi zao 59 wakiiacha nyuma ya pointi 11 mtani wake Yanga Sc.

Kikosi cha kwanza cha Simba hata mtoto mdogo ukimpa akupangie atakutajia kuanzia mlinda mlango hadi winga wa kucheza namba 11, na pia atakutajia wachezaji wanaokaa benchi, kwa vyovyote Mohamed Ibrahim "Mo" atakuwa jukwaani akiufuatilia mpira huo.

Siku nyingi sana sijamuona Mo Ibrahim akiwa ameuvalia ule uzi wa rangi nyekundu na micharazo meupe mabegani, Mo sijamuona hata benchi akisubiri kuchukua nafasi aingie, tayari mashabiki wameshamsahau.

Ilikuwa ngumu mashabiki wa Simba kumsahau Jonas Mkude, walipiga ukelele kwa kocha wao Mcameroon, Joseph Omog, na walipoona hampi sana nafasi Mkude wakamchongea kwa viongozi na mwishowe akaletewa msaidizi Mrundi Masoud Djuma Irambona kisha baadaye akafutwa kazi mazima.

Mashabiki wa Simba walimpenda sana Mkude kuliko kocha Omog na ndio maana alipotimuliwa Omog furaha iliongezeka, walijua mchezaji wao wanayempenda atacheza, hivyo ndivyo ilivyo kwa Mohamed Ibrahim "Mo" naye alihusudiwa na mashabiki wa Simba.

Lakini kwa sasa mashabiki hao hao wa Simba wametulia na hawapigi tena kelele za kumtaka Mo acheze, na ndio maana iko kimya sana sauti ya kumtaka Mo acheze, na ukimya wake umezidi kumpoteza kabisa kisoka.

Hakuna mtu anayemtaka Mo kwa sasa, na wanaelekea kwenye mchezo wao na Yanga Mo hayumo wala hazungumzwi, maisha yanakuwa magumu sana kwake, lakini kabla hajaongezewa mkataba na Simba, taarifa za kutakiwa na mahasimu Yanga zilisambaa.

Inasemekana Yanga walikuwa wakimuhitaji kwa udi na uvumba, Mo bado ni mchezaji mzuri na kama anapewa nafasi basi anaweza kuonyesha vitu vyake, lakini kwa ubora unaoonyeshwa na wachezaji wa Simba sidhani kama kuna namba yake.

Kocha mkuu wa Simba, Mfaransa Pierre Lechantre na msaidizi wake Masoud Djuma Irambona nawaona wako sahihi na kikosi chao, hawana upendeleo wowote kwa wachezaji wao, wanawapanga kutokana na kile qanachokifanya uwanjani, na ndio maana Simba inaongoza ligi.

Wekundu wa Msimbazi wanaongoza ligi wakiwa na pointi 59 na mechi 25 wakifuatiwa na Yanga Sc wenye pointi 47 na mechi 23, isipokuwa Yanga ana mechi zake mbili za viporo hajacheza kwa maana hiyo kama akicheza na kushinda anaweza kubakiza gepu la pointi 5 hivyo Jumapili itakuwa mechi ngumu.

Simba watacheza kwa jihadi na wakiingia uwanjani kwa kutegemea kikosi chao cha kwanza ambapo Mo Ibrahim hatokuwepo, Dirisha la usajili litagunguliwa tena Juni mwaka huu hasa baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu bara msimu wa 2017/18.

Hivyo wachezaji ambao mikataba yao inamalizika na hawana msaada wanaachwa waende kwingineko, na wale ambao mikataba yao bado haijakwisha na hawana msaada wanatolewa kwa mkopo, msaada wa Mo Ibrahim ndani ya Simba kwa sasa siuoni kabisa hivyo itakuwa jambo la busara kama viongozi wa Simba na benchi zima la ufundi wakamtoa kwa mkopo nyota huyo ili akaonyeshe kiwango chake kwingineko.

Mwisho namalizia kuwa Mo Ibrahim ni hazina ya taifa hivyo kama atakuwa anacheza katika kiwango chake kilekile tulichomzoeaga kuanzia Mtibwa Sugar na Simba Sc bila shaka ataitwa na timu ya taifa, Taifa Stars na kuisaidia nchi yetu

Alamsiki

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC