Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU

: NI ASANTE KWASI, ANAYETEMBEA NA UBINGWA WA SIMBA.

Na Prince Hoza

Simba Sc ina muunganiko mzuri kuanzia sehemu ya ulinzi, kiungo hadi ushambuliaji, na hiyo ndiyo imeifanya klabu hiyo iliyozaliwa mwaka 1936 kuongoza ligi kwa tofauti kubwa ya pointi baina yake na wanaomfuatilia.

Kasi ya Simba imezidi kuongezeka katika mzunguko wa pili, Simba inaongoza ligi ikiwa na pointi 42 ikicheza mechi zake 18 pamoja na ule wa jana dhidi ya Mwadui Fc ulioisha kwa sare ya 2-2 uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga.

Vinara hao wamewaacha mbali wapinzani wake Yanga, Azam na Singida United ambao wanawafuatilia kwa nyuma, kikosi hicho kinachonolewa na Mfaransa, Pierre Lechantre na msaidizi wake Masoud Djuma raia wa Burundi kimeonekana kuwa imara msimu huu na kinaweza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Chachu ya ushindi iliyopo katika klabu ya Simba haiji bure isipokuwa inatokana na ushirikiano mkubwa uliopo kwa wachezaji wa kikosi hicho, miongoni mwa wachezaji tegemeo ni Asante Kwasi raia wa Ghana.

Anapokosekana Kwasi, Simba inapungua makali kama ilivyotokea jana ilipokubali sare ya 2-2 na vijana wa Mwadui, Kwasi ni chaguo la Simba msimu huu akisajiliwa wakati wa usajili wa Dirisha dogo la Desemba mwaka jana, Kwasi ni beki mwenye uwezo wa kucheza pembeni na katikati, lakini pia anaweza kucheza kama kiungo mkabaji au mshambuliaji.

Alianza kufahamika msimu uliopita alipokuwa anaichezea Mbao Fc ya jijini Mwanza, Kwasi alikuwa mmoja wa wachezaji walioipa kiburi timu hiyo ambayo iliweza kuzivimbia Simba na Yanga, timu hiyo pia iliweza kuingia fainali ya kombe la Azam Sports Federation Cup na ikakutana na Simba Sc katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Kwa bahati mbaya Mbao Fc ikachapwa mabao 2-1 lakini mchezo ulikuwa mkali na wa kusisimua ulioudhuriwa na Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Mhe Kassim Majaliwa.

Asante Kwasi hakuwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa midomoni mwa mashabiki wa soka nchini, hata vilabu vikubwa vya Yanga, Simba na Azam havikumfikiria hata kidogo, jina lililokuwa likihubiriwa sana ni la Yusuf Ndikumana ambaye alionekana kama beki bora wa Mbao Fc.

Ndikumana aliwaniwa na vilabu vitatu hivyo vyenye mashabiki wengi na ukwasi mkubwa wa noti, lakini mwishowe Ndikumana akasalia Mbao Fc hasa baada ya kuona anatakiwa kwa dau dogo wakati yeye ni staa wa Mbao Fc.

Kwasi alionekana si lolote si chochote ni mchezaji wa kawaida sana, hakutikisa kwenye vichwa vya habari vya magazeti yetu ya michezo hapa nchini, mzaliwa huyo wa Ghana aliyezaliwa miaka 25 iliyopita akaachwa aende zake, kijana wa watu akajiunga na Lipuli Fc ya Iringa timu iliyopanda Ligi Kuu msimu huu.

Simba yenyewe iliishua kumuona Emmanuel Mseja, wakati Yanga Sc ikamuona Pius Buswita, na Azam Fc ikamnasa Salmin Hoza, na hao ndio wakaonekana wachezaji bora wa Mbao Fc mpaka kusajiliwa na klabu kubwa za hapa Tanzania, Asante Kwasi akiwa na Lipuli yake aliweza kuisaidia timu hiyo kupambana na hatimaye ikavivimbia vigogo Yanga na Simba.

Lipuli ilianza kuibana Yanga katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam ikitoka nayo sare ya bao 1-1, Kwasi alionekana kuwa kikwazo kwa Yanga, hasa baada ya kumdhibiti vilivyo kiungo wa mabingwa hao watetezi, Mkongoman, Papy Kabamba Tshishimbi.

Kwasi pia akaishika na Simba baada ya Lipuli kutoka nayo sare ya 1-1 uwanja wa Uhuru pia, beko huyo aliisawazishia Lipuli kwa goli lake zuri la kichwa, kuanzia hapo Simba walianza kumvizia na kisha wakafanikiwa kumsajili moja kwa moja kwa ada ya shilingi Milioni 25 za Kitanzania.

Beki huyo anayesifika kwa upachikaji, hadi anahamia Msimbazi alikuwa amefunga magoli matano, na alipoanza kazi Simba akafanikiwa kufunga bao moja na sasa ana mabao sita akichuana vikali na washambuliaji Ibrahim Ajibu wa Yanga, Shiza Kichuya wa Simba, Marcel Boniventure wa Majimaji na Mohamed Rashid wa Tanzania Prisons wenye mabao sita kila mmoja.

Na kwa uchezaji wake kwa vyovyote anaweza kabisa kuipa taji la 19 Simba Sc msimu huu wa 2017/18, Simba imekosa ubingwa wa Bara zaidi ya misimu mitatu, Asante Kwasi pia amewahi kuichezea Mbabane Swallors ya Swaziland timu ambayo pia alikuwa akiichezea kiungo wa Yanga, Mkongoman Papy Kabamba Tshishimbi

Asante Kwasi

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC