Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BOCCO AWA MWANASOKA BORA WA MWEZI JANUARI, VPL

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Nahodha na mshambuliaji wa vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba Sc, John Raphael Bocco "Adebayor" ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Januari wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Bocco ameshinda tuzo hiyo baada ya kufanikiwa kuwashinda Emmanuel Okwi pia wa Simba na Awesu Awesu wa Mwadui Fc, mshambuliaji amefanya vizuri katika mwezi Januari na kuisaidia timu yake kushinda mechi tatu akishiriki kikamilifu kwa mechi zote.

Kwa mujibu wa kamati ya tuzo kwa kushirikiana na makocha, wamejiridhisha kumpa Bocco tuzo hiyo hasa baada ya kuimarika kwa kiwango, hadi sasa Bocco amefunga jumla ya mabao tisa akishikilia nafasi ya tatu.

Tuzo hiyo msimu huu ilianza kwenda kwa Mganda Emmanuel Okwi aliyeshinda Agosti, Septemba ilienda kwa Shafik Batambuze naye ni Mganda wakati Oktoba ilienda kwa Mzambia Obrey Chirwa.

Wengine walioshinda tuzo hiyo ni Mudathir Yahya mwezi Novemba na Habibu Kiyombo aliyeshinda mwezi Desemba, Bocco sasa atajinyakulia kisumbuzi kutoka Azam pamoja na kitita cha shilingi Milioni moja.

John Bocco "Adebayor" ameshinda tuzo ya mwanasoka bora wa Vpl 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...