BOCCO AWA MWANASOKA BORA WA MWEZI JANUARI, VPL

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Nahodha na mshambuliaji wa vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba Sc, John Raphael Bocco "Adebayor" ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Januari wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Bocco ameshinda tuzo hiyo baada ya kufanikiwa kuwashinda Emmanuel Okwi pia wa Simba na Awesu Awesu wa Mwadui Fc, mshambuliaji amefanya vizuri katika mwezi Januari na kuisaidia timu yake kushinda mechi tatu akishiriki kikamilifu kwa mechi zote.

Kwa mujibu wa kamati ya tuzo kwa kushirikiana na makocha, wamejiridhisha kumpa Bocco tuzo hiyo hasa baada ya kuimarika kwa kiwango, hadi sasa Bocco amefunga jumla ya mabao tisa akishikilia nafasi ya tatu.

Tuzo hiyo msimu huu ilianza kwenda kwa Mganda Emmanuel Okwi aliyeshinda Agosti, Septemba ilienda kwa Shafik Batambuze naye ni Mganda wakati Oktoba ilienda kwa Mzambia Obrey Chirwa.

Wengine walioshinda tuzo hiyo ni Mudathir Yahya mwezi Novemba na Habibu Kiyombo aliyeshinda mwezi Desemba, Bocco sasa atajinyakulia kisumbuzi kutoka Azam pamoja na kitita cha shilingi Milioni moja.

John Bocco "Adebayor" ameshinda tuzo ya mwanasoka bora wa Vpl 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI