Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ALIYEVUMA

RAMADHAN LENNY, KIUNGO BORA ALIYEPITA MSIMBAZI.

Na Shafih Matuwa

Jina la Ramadhan Lenny Maufi si geni masikioni mwa wapenzi wa mpira wa miguu hapa nchini hasa wale wa miaka ya 90, kwa vijana wa kileo inawezekana ikawa changamoto kumfahamu.

Na ndio maana Mambo Uwanjani imeamua kuwaletea makala fupi ya kuwakumbusha nyota waliopata kutamba huko nyuma tena wale WALIOVUMA.

Leo hii tumemmulika kiungo fundi kabisa ambaye inasemekana hajawahi kutokea katika kikosi cha Simba kwa misimu yote tangia ilipoanzishwa mwaka 1936, si mwingine ni Ramadhan Lenny Maufi ambaye kwa sasa ni marehemu.

Lenny alikuwa kiungo mkabaji namba sita ambaye hakuna mfano wake tena, hata hao akina Seleman Matola, Jonas Mkude na wengineo hawamfikii.

Lenny amekufa na ubora wake, aliisaidia Simba kutamba katika ngazi mbalimbali za ndani na nje, Simba kuchukua ubingwa wa Bara haikuwa shida kama ilivyo sasa inasotea mwaka wa tano huu haijachukua.

Simba ilikuwa ikitwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya muungano wakati huo ilikuwa ikichezwa kwa kushirikisha timu tatu za juu kutoka bara na tatu za juu kutoka visiwani.

Wakati huo wachezaji wa Kitanzania walikuwa na soko katika falme za Kiarabu, hivyo Lenny alikuwa akienda mara kwa mara kucheza soka la kulipwa aidha Oman au Dubai, Waarabu walikuwa wanamkubali sana.

Fundi huyo wa mpira ambaye mdogo wake alikuwa akiichezea Pilsner ya Dar es Salaam, Kaingilila Lenny Maufi, kwa hakika atakumbukwa hasa pale alipoisaidia Simba kutwaa ubingwa wa vilabu Afrika mashariki na kati sasa kombe la Kagame mara mbili mfululizo.

Pia Lenny alikuwemo kwenye kile kikosi kilichoingia fainali ya kombe la CAF mwaka 1993 Simba ilicheza na Stella Abidjan katika uwanja wa Taifa sasa Uhuru na kufungwa mabao 2-0.

Kimetajwa kikosi bora cha Simba cha muda wote kuwahi kutokea, Lenny ameonekana ndiye namba sita bora, ukimtazama huwezi kuamini vitu vyake uwanjani, ana utege flani hivi miguu kutokelezea kwa ndani, duh lakini balaa, akiunasa mpira hatari

Ramadhan Lenny (Katikati) anatajwa kama kiungo bora Simba Sc

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC