Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU

SHOMARI KAPOMBE. AMERUDI KUWASHIKA.

Na Prince Hoza

MCHEZAJI ambaye sikutaka asajiliwe na Simba msimu huu ni Shomari Kapombe, kitu pekee kilichonifanya nisipende asajiliwe ni majeruhi aliyonayo ambayo nilidhani kama yatamfanya asirejee katika ubora wake.

Ama kweli nililaani sana usajili wa Kapombe mpaka kufikia kumshutumu mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu ya Simba, Kapteni mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ). Zacharia Hanspoppe, sikuona mantiki yoyote Simba kumuacha Mkongoman Janviel Bokungu na kumsajili kiungo huyo mwenye uwezo pia wa kucheza  kama beki.

Kapombe ni mchezaji mzuri na ndio maana akapata nafasi ya kwenda kucheza soka la kulipwa nchini Ufaransa katika klabu ya Cannes inayoshiriki Ligi Daraja la nne.

Lakini tatizo kubwa linalomsumbua maishani mwake ni maumivu ya nyonga, inafikia wakati Kapombe anatamani kuachana na soka na kufanya shughuri nyingine, Kapombe amekosa raha kwa kipindi kirefu hasa akiwa nje ya uwanja akiuguza majeraha yake.

Nyota huyo alisajiliwa na Simba mwanzoni mwa msimu huu akitokea Azam Fc na tangu alipotua Simba hakuwa na mwanzo mzuri kwani alishindwa kuitumikia klabu yake baada ya kutonesha jeraha lake akiwa kwenye mazoezi ya timu ya taifa, Taifa Stars.

Kapombe aliumia mazoezini wakati Stars ikijiandaa kushiriki michuano ya COSAFA CASTLE CUP iliyofanyika nchini Afrika Kusini, baada ya kuumia, Kapombe alikuwa akipatiwa matibabu yaliyomweka nje kwa kipindi cha miezi mitano.

Alikosa mechi 12 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, michuano ya FA na kombe la Mapinduzi na pia alikosa mechi ya kuwania Ngao ya Jamii na zile za maandalizi ya msimu, kwa bahati nzuri beki huyo amerejea uwanjani na nwanzoni mwa wiki hii aliichezea Simba kwa mara ya kwanza ilipoumana na Kagera Sugar, mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Kapombe aliingia kipindi cha pili akichukua nafasi ya Mghana, Nicolaus Gyan na kuweza kuonyesha kwamba yeye bado ni mchezaji bora isipokuwa majeraha tu ndio yaliyokuwa yakimtesa, mchezo huo uliofanyika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Simba ilishinda mabao 2-0.

Kapombe alihusika kuseti bao la pili baada ya kuingia nao mpira hadi karibu ya lango la Kagera Sugar na kumpasia nahodha John Raphael Bocco "Adebayor" aliyeuweka kimiani na kumuacha kipa mkongwe Juma Kaseja asijue la kufanya na kuwa bao la pili huku goli la kwanza likifungwa na kiungo Said Ndemla.

Kapombe alikaribia kuseti lingine lakini Emmanuel Okwi alichelewa, huyo ndiyo Shomari Salum Kapombe aliyezaliwa mjini Morogoro Januari 28, 1992 na kuanza kuonyesha kipaji chake katika timu ya Morogoro Youth Academiya kabla ya kujiunga na Polisi Moro.

Nyota yake ilianza kung' ara alipokuwa kwenye timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 iliyokuwa ikinolewa na Jamuhuri Kihwelo "Julio" ambapo timu hiyo iliweza kutamba katika michuano ya kufuzu mataifa Afrika kwa vijana na ndipo klabu ya Simba ilipoamua kumsajili.

Kapombe alianza kuichezea Simba kuanzia msimu wa 2011 hadi 2013 alipoenda nchini Ufaransa kucheza soka la kulipwa katika timu ya Cannes, alijiunga na timu hiyo msimu wa 2013/14 hakudumu sana akarejea nyumbani Tanzania.

Mwaka huo huo 2014 alijiunga na Azam Fc ambapo alidumu nayo hadi mwaka 2017 aliporejea Simba, Ki- Asilia Kapombe ni kiungo lakini ana uwezo pia wa kucheza karibu nafasi zote uwanjani sijui kipa, na anajulikana kama kiraka.

Katika orodha ya mabeki wanaofunga, sifa ambayo anayo Mghana, Asante Kwasi,  Shomari Kapombe naye anayo kwani anasifika kwa kufunga na kutengeneza nafasi ya kufunga, Kapombe amewahi kuwemo katika orodha ya wafungaji bora wakati huo alipokuwa anaichezea Azam Fc.

Kapombe aliingia kwenye mzozo na mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu ya Simba, Zacharia Hanspoppe hasa kuhusu kucheza, Hanspoppe alidai beki huyo amepona ila hataki kucheza na akamtaka achague moja kucheza au kuondoka.

Lakini mlinzi huyo alimjibu Hanspoppe kuwa yeye hajapona na hawezi kucheza mpaka atakapopona ila kama Simba wako tayari kumlipa pesa zake basi wavunje mkataba naye, hata hivyo mzozo huo uliishia kwenye vyombo vya habari na mchezaji huyo aliendelea na tiba mpaka kuruhusiwa na daktari wa kkabu ya Simba, Yassin Gembe.

Jumatatu iliyopita Kapombe alidhihirisha ubora wake alipochangia goli ka pili na la ushindi kwa Simba Sc ambao ni vinara wa ligi hiyo kwa pointi 32 huku nyuma yake ipo Azam Fc yenye pointi 30, Kapombe ni kama amerudi kuwashika wale waliokuwa hawamwamini nikiwemo mimi

NAWATAKIA IJUMAA KAREEM, TUKUTANE JUMA LIJALO

Shomari Kapombe (Kushoto) akiwa na kocha msaidizi wa Simba, Masoud Djuma

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...