Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga yakwama kwa Prisons, Simba washindwe wenyewe

Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam

Licha ya kucheza pungufu, vijana wa Tanzania Prisons jioni ya leo wamefanikiwa kuwabana mbavu wakongwe Yanga SC na kutoka nao sare ya kufungana bao 1-1 katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya jiji la Dares Salaam, mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Endapo Yanga ingeibuka na ushindi leo ingefanikiwa kukamata kiti cha usukani wa ligi kwani ingefikisha pointi 23 ikiziacha nyuma Simba na Azam zenye pointi 22 kila moja, hata hivyo sare hiyo imewapa pointi moja sasa wamefikisha pointi 21 wakiendelea kukaa katika nafasi yao ya tatu.

Prisons walikuwa wa kwanza kupata bao la uongozi likifungwa kipindi cha kwanza dakika ya 10 na mshambuliaji wake Eliud Mpepo lakini Yanga wakachomoa kupitia Raphale Daudi.

Prisons walionekana kuelemewa zaidi na kupelekea wachezaji wake kujiangusha hovyo na kupoteza muda, Ligi hiyo iliendelea katika viwanja vingine tofauti ambapo Ruvu Shooting ilishinda 2-1 dhidi ya Majimaji ya Songea uwanja wa Mabatini Mlandizi.

Hata hivyo mwamuzi wa mchezo huo aliwanyima Yanga bao la wazi kabisa lililofungwa na Obrey Chirwa aliyemalizia mpira uliotemwa na kipa wa Prisons, lakini mwamuzi alikataa akidai mfungaji ameotea.

Kagera Sugar na Stand United zilitoka sare 0-0 uwanja wa Kaitaba, Bukoba wakati Mbao FC ikiifunga Mwadui FC 1-0, CCM Kirumba Mwanza, ligi itaendelea kesho kwa mechi moja Simba SC na Lipuli uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam

Yanga wamelazimishwa sare na Prisons leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...