BOCCO AZIMA NGEBE ZA WAJELAJELA

Na Exipedito Mataruma. Mbeya

Goli lililofungwa kunako dakika ya 85 na mshambuliaji John Rafael Bocco "Adebayor" limetosha kabisa kuipa pointi tatu Simba SC baada ya kuilaza Tanzania Prisons bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Mchezo huo uliomalizika jioni hii ulikuwa mkali na wa kusisimua na kila timu ilijaribu kupeleka mashambulizi langoni kwa mwenzie, mechi hiyo ngumu imefanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Edward Moringe Sokoine jijini Mbeya na Simba kuweza kujizolea pointi sita na sasa ikifikisha pointi 22 ikiwa imeshuka uwanjani mara kumi.

Mchezo wa leo umekumbushia ule wa msimu uliopita uliofanyika katika uwanja huo huo wa Sokoine ambapo vijana wa Prisons waliweza kuchomoza na ushindi wa mabao 2-1 yaliyofungwa na Victor Hangaya ambaye kwa sasa amejiunga na Mbeya City

John Rafael Bocco amezima ngebe za Prisons leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI