Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU:

IBRAHIM CLASS. MTANZANIA WA KWANZA KUTWAA UBINGWA WA NDONDI WA GBC WA DUNIA.
Na Prince Hoza
NAKUMBUKA kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kilipata mapokezi makubwa wakati kilipowasili nchini kikitokea Afrika Kusini ambako kilienda kushiriki michuano ya COSAFA Castle Cup.
Taifa Stars ilikamata nafasi ya tatu ambapo ilitunukiwa medali ya shaba na kitita cha fedha, Dola 10,000 za Kimarekani, Stars ililakiwa na waziri wa habari, michezo, sanaa na utamaduni, Dk Harrison Mwakyembe kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa Mwl Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.
Na pia aliweza kuzungumza na wachezaji wa timu hiyo akiwapongeza kwa hatua hiyo waliyofikia huku pia akiwataka waongeze bidii na waweze kuishinda Rwanda katika mchezo wao uliofuata wa michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani, maarufu CHAN.
Mwakyembe amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha timu yetu ya taifa inafanya vizuri kwani hiyo si mara yake ya kwanza, alishafanya hivyo mara kadhaa zilizopita wakati alipochaguliwa kuongoza wizara hiyo na mheshimiwa Rais, Dk John Magufuli, aliwahi pia kuhamasisha hivyo kwa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Serengeti Boys ambayo ilishiriki fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) kwa vijana wa umri huo nchini Gabon mwaka huu.
Vijana hao wa Serengeti Boys walipokewa kwa halaiki ya viongozi wa kiserikali akiwemo waziri Mwakyembe ambaye ana dhamana kubwa kwenye upande wa michezo, ikimaanisha michezo yote, lakini walimsahau Mtanzania mwingine anayefahamika kwa jina la Ibrahim Class au King Class ambaye naye alitoka kuipeperusha vema bendera ya Tanzania nje ya mipaka yetu.
Ibrahim Class yeye ndiye ameitoa kimasomaso Tanzania naweza kusema kwa mwaka huu 2017 baada ya kufanikiwa kutwaa mkanda wa dunia wa Global Boxing Council (GBC) akimchakaza bondia Jose Ferero wa Panama mchezo ambao ulifanyika nchini Ujerumani na kuweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kutwaa mkanda huo.
Ubingwa wa dunia ni heshima tosha kwa Tanzania lakini bondia huyo anayepigania uzani wa Light Middle Kg 61 hakupata hamasa yoyote kutoka serikalini wala kwenye chama chochote cha ndondi hapa nchini, zaidi ya meneja wake ambaye alimsaidia kumfikisha hapo halipo.
BONDIA IBRAHIM CLASS (KATIKATI) AKIONYESHA MKANDA WAKE.

Class anayenolewa na Habibu Kinyogoli na Rajabu Mhamila maarufu Super D, ana mafanikio makubwa kwenye mchezo huo kwani licha ya kutwaa ubingwa wa dunia wa GBC, Pia anashikilia mkanda wa UBO Afrika ambao aliutwaa baada ya kumchakaza Mtanzania mwenzake Cosmas Cheka.

Ibrahim Class si bondia wa kumbeza kwani ameitoa kimasomaso Tanzania kwani alitwaa mkanda mwingine wa kimataifa wa WPBF kwa kumpiga bondia wa Zambia Mwansa Kabinda kwa TKO, hayo ni mafanikio makubwa kwa mwanamichezo huyo ambaye alipaswa japo kupongezwa na kupewa heshima yake ikiwemo serikali kumpa hamasa kama inavyofanya kwenye soka na riadha.

Ibrahim Class aliyezaliwa miaka 26 iliyopita, ana rekodi ya kucheza mapambano 22 na 18 ameweza kushinda huku manne pekee amepoteza, kitu kikubwa ambacho Class amekisema ni kuhusu yeye kujituma na ndio kumempa mikanda yote hiyo.

Anasema amekuwa akifanya mazoezi ya nguvu kuanzia asubuhi na jioni, pia anammwagia sifa meneja wake kwa kumsaidia na kumfikisha hapo halipo huku akiwaahidi Watanzania kwamba atafikia levo za akina Manny Paquiano au Froiyd Maywether kwani wote hao anawahusudu mno.

Class, mbali na kufanikiwa kuwafikia akina Rashid Matumla "Snake Boy" , Francis Cheka kwa maana ya rekodi zao, lakini amedai amesahaulika sana na anaona kama Tanzania inathamini soka peke yake huku michezo mingine kama ndondi ambayo inaitangaza vema nchi ikiachwa.

Mchezo wa soka umekuwa ukiigharimu nchi fedha nyingi lakini kila kukicha ukizidi kuporomoka, hivi karibuni Shirikisho la mpira wa miguu duniani (Fifa) ulitoa orodha ya ubora wa viwango kwa timu za taifa, ambapo Tanzania ilianguka kutoka nafasi ya 125 hadi 136

BONDIA IBRAHIM CLASS NA MKANDA WAKE WA GBC

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC