Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KISPOTI:

SIKUBALIANI NA LIGI KUU KUWA NA TIMU 20 MSIMU UJAO.

Na Prince Hoza

KWANZA kabisa nianze kwa kuupongeza uongozi mpya wa Bodi ya Ligi (TPLB) uliochaguliwa Oktoba 15 mwaka huu, pongezi sana Kaimu mwenyekiti wa Yanga SC, Clement Andrew Sanga kwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Bodi hiyo.

Lakini pia shukrani zangu nyingine nazielekeza kwa makamu mwenyekiti mpya wa Bodi hiyo, Shani Christoms Mrigo pamoja na wajumbe waliochaguliwa kuunda kamati ya Bodi hiyo ambayo itakuwa ikisimamia kutoa maamuzi mbalimbali yanayohusu ligi.

Ikumbukwe Bodi ya Ligi inasimamia Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL), Ligi Daraja la kwanza Tanzania bara (FDL) na Ligi Daraja la pili Tanzania bara (SDL).

Kupatikana kwa uongozi huo mpya wa Bodi ya Ligi kunakamilisha mchakato mzima wa uchaguzi na pia kunadhihirisha sasa kuwa mambo mapya yanaanza, tayari Shirikisho la mpira wa miguu nchini, (TFF) limeshapata viongozi wake wapya baada ya Jamal Malinzi na wenzake kukamilika kwa kipindi chao cha uongozi.

TFF ilipata Rais wake mpya ndugu Wallace Karia na makamu wake, Michael Wambura, bila shaka viongozi wa TFF na wa Bodi ya Ligi wataweza kushikamana na kuuendeleza mpira wa Tanzania, kitu ambacho ningependa kipewe kipaumbele kwa sasa ni kuiboresha Ligi Daraja la kwanza.

Na kitu kinachonishangaza ni pale niliposikia kwamba msimu ujao Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara itashirikisha jumla ya timu 20, na msimu huu jumla ya timu mbili zitatelemka daraja badala ya tatu kama ilivyozoeleka.

Sipingani hilo isipokuwa sikubaliani na mpango huo kwa maana bado tuna safari ndefu kuelekea huko, Shirikisho letu la mpira wa miguu (TFF) na Bodi yetu ya ligi bado havijaweza kuonyesha ufanisi wao kikazi na inahitaji muda kidogo ili waweze kuaminiana.

Bodi ya Ligi ndio wenye kuendesha na kusimamia Ligi zote tatu ambazo ni kubwa kwa hapa nchini na ndio wenye majukumu ya kupitia mechi zote za mashindano hayo, lakini TFF imekuwa ikiingilia kazi za Bodi ya Ligi kiasi kwamba zimekuwa zikigongana.

Tulijionea msimu uliopita ambapo Shirikisho hilo lilipotengua maamuzi ya kamati ya masaa 72 ambayo ni ya Bodi ya Ligi, hapo utaona jinsi vyombo hivyo vinavyoingiliana, ningefurahi kama TFF ingevunja kamati yake ya mashindano ili kamati hiyo ihamie Bodi ya Ligi kwakuwa wao ndio wenye ligi na TFF ni msimamizi tu.

Nikija na hili la timu 20 kushiriki Ligi Kuu bara msimu naliona gumu na sidhani kama litaenda sambamba na maendeleo ya mpira wetu, tatizo kubwa linalopelekea mimi kuingia wasiwasi ni ratiba yetu ya nchi kwa mashindano yote.

Ligi inayoshirikisha timu 16 inachukua miezi tisa kumalizika, hapo bado hakujafanyika michuano ya Chalenji wala klabu Afrika mashariki na kati, hakujafanyika michuano ya kombe la Mapinduzi ambayo nayo husimamisha ligi, bado mashindano kama ABCBank ambayo yalifanyika mara moja tu hajafanyika tena.

Ratiba yetu itakuja kuumbua hili la timu 20 ambayo sasa nahisi inaweza kuchezwa mwaka mzima, TFF kama eangejikita kutengeneza vizuri mfumo wa soka letu halafu Bodi ya Ligi ikacheza na kalenda ili masuala ya kuhairisha mechi ama kusogeza mbele mechi isingekuwepo.

Hakuna haja kusogeza mbele mechi za ligi kama kalenda ya FIFA, tunayo, kalenda ya CAF tunayo, kalenda ya CECAFA tunayo nadhani hapo kungesaidia kupanga rariba nzuri za ligi zetu ambazo hazitaingiliana na kalenda za mashirika hayo makubwa ya mpira.

Tatizo tulilonalo Watanzania kujifanya tunajua wakati hatujui, tumekuwa wanafikiwanafiki, hatuwezi kusimamia ukweli, na ndio maana tumekuwq tukikubali kila tunachoambiwa na bwana mkubwa, kulikuwa hakuna umuhimu wowote wa kukubali timu 20 zicheze Ligi Kuu msimu ujao.

Ligi Daraja la kwanza ndiyo iliyohitaji maboresho, haiwezekani ikaitwa Ligi Daraja la kwanza halafu ikachezwa kwa makundi, hilo nalo ni tatizo, haiwezekani hadhi iliyonayo Ligi Daraja la kwanza ikachezwa bila kuwepo mdhamini ambaye angezisaidia timu hizo kusafiri eneo moja kwenda lingine kushiriki ligi hiyo.

Maboresho Ligi Daraja la kwanza yakifanikiwa kwa asilimia 70 hapo sasa uwezekano wa kuongeza timu Ligi Kuu bara ungefanyika, lakini pia bado tunahitaji mabadiliko zaidi kwenye uendeshaji wa Ligi Kuu na tatizo hilo tungetaka lisijirudie.

Haiwezekani Ligi Kuu isimame wiki nzima kupisha timu ya taifa icheze mchezo wa kirafiki, ilipaswa ligi ichezwe angalau katikati ya wiki halafu mwishoni ikacheza timu ya taifa, hili bado tatizo na mnataka kuongeza tatizo, tutaona msimu ujao Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania ikichezwa mwaka mzima.

Tukutane tena Jumatatu ijayo,nawatakia mchezo mwema wa Simba na Yanga Jumamosi ijayo ya Oktoba 28, 2017 ALAMSIKI

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC