Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SOPHIA ABDUL "KIBENA": NYOTA MPYA KWENYE FILAMU, AAPA KUMFIKIA WEMA SEPETU

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazopiga hatua kwenye tasnia ya filamu Duniani, tofauti na miaka iliyopita ambapo kulikuwa na wasanii wachache kwenye fani hiyo.

Lakini sasa kila kona kumetapakaa vikundi vya sanaa huku kampuni za kutengeneza filamu zikizidi kuongezeka, vijana wa kike na kiume nao wanajikita kwa wingi kwenye tasnia hiyo, tofauti na miaka ya nyuma ambapo ilikuwa vigumu kuwaona vijana wakiigiza.

Miaka hiyo wazee pekee ndio waliotawala kama mzee Jangala, mzee Jongo (Marehemu), Bi Hambiliki (Naye marehemu), mzee Kagunga, mzee Janja, Bi Hindu, mzee Kipara, mzee Mahoka, mzee Pwagu, mzee Panda, mzee Majuto, mzee Small na wengineo waliweza kushiriki maigizo.

King Majuto ama mzee Majuto na mzee Small wao ndio walifungua milango kwa kufanikiwa kutengeneza filamu ambazo zilisisimua wengi na kuanza kuwavutia vijana ambao nao walianza kujiingiza kwenye tasnia hiyo, marehemu Steven Kanumba, Elizabeth Michael "Lulu", Aunt Ezekiel, Irene Uwoya, Wema Sepetu na wengineo nao waliweza kuwavuta vijana zaidi na sanaa kuzidi kutanuka.

KIKUNDI CHA NEW HOPE AMBACHO SOPHIA ANAKITUMIKIA.
.......
Mwanadada Sophia Abdul Ramadhan Kinyogoli maarufu Kibena ni miongoni mwa wasanii waliojikita kwenye filamu, Sophia yeye aliingia kwenye tasnia hiyo mwaka 2015 akiwa anasoma Kibaha, na anasema aliipenda sana sanaa hiyo mpaka akaamua kuacha shule.

Sophia anasema aliacha shule akiwa kidato cha pili na akaamua kuondoka Kibaha na kuja jijini Dar es Salaam ambapo amepokewa na baba yake mdogo pamoja na mama yake mdogo ambao anaishi nao kwa sasa maeneo ya Kawe.

Aliamua kuendelea na sanaa ambapo anamtaja kaka mmoja anayejulikana kwa jina la Gebo ndiye aliyemtafutia kikundi cha sanaa na akaungana nacho, Sophia anasema alikutana na Gebo kwenye mtandao wa facebook ambapo waliunganishiana dili humo humo.

Anasema kundi lake la kwanza lilikuwa linaitwa Chamazi Arts lililopo Mbagala Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, lakini aliishia kufanya mazoezi mpaka mwaka 2016 alipotafutiwa kikundi kingine, anasema hakuwahi kukutana na kamera zaidi ya kufanya mazoezi matupu.

Anadai kundi lake hilo ka kwanza kulitokea malumbano na wenzake hivyo akaamua kuachana nalo, anasema wakati siku zilivyozidi kusogea mbele na yeye akawa anazidi kuimarika na akawa mmoja kati ya wasanii mahiri kwenye sanaa hiyo.
SOPHIA (WA PILI KUTOKA KUSHOTO) AKIWA NA WASANII WENZAKE.

Anasema akiwa ametulia nyumbani alipigiwa simu na mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Komba ambaye anaishi Buguruni Dar es Salaam, ambapo alimjulisha kuwa anahitajika maeneo ya Mwananyamala akajiunge na wasanii wenzake waliokuwa chini ya staa Big Matovolwa ili warekodi tamthilia.

Anakiri kuwa hakuamini moyoni mwake kama kweli anahitajika kurekodi kwani hakuwahi kurekodi hata mara moja, lakini aliweza kushiriki vema kwenye tamthilia hiyo kwani wenzake walimsifia sana na kumtia moyo.

Baada ya kushiriki tamthilia hiyo akapata nafasi nyingine ya kushiriki tamthilia nyingine, safari hii akiitwa na kijana mwingine aitwaye Shafih ambaye alimpeleka katika kikundi cha New Hope kilichopo Tandale Dar es Salaam, anasema alifanyiwa usaili na akakubalika.

Sophia analitaja kundi hilo kuwa ndio limefungua njia yake ya kuelekea kutimiza ndoto yake ya muda mrefu ya kuwafikia mastaa kama Wema Sepetu ambao alikuwa akiwaona tu kupitia televisheni, akiwa na New Hope, Sophia anashiriki katika tamthilia yao ya Msitu wa Ndendemba ambayo inarushwa katika kituo cha runinga cha SIBUKA, Sophia anasema yeye alizaliwa miaka 20 iliyopita mjini Kibaha mkoani Pwani.

Anasema yeye ni mwenyeji wa Mlandizi mkoani Pwani na amekuwa akivutiwa zaidi na Wema Sepetu na Gabo na siku moja alitamani kufanya nao kazi angalau mara moja, Sophia anasema katika maisha yake amewahi kukutana na misukosuko ikiwemo ya kutoa mimba aliyopachikwa akiwa na miaka 16.

Ameongeza kuwa hata mama yake mzazi hataki kusikia yeye akijihusisha na sanaa na ndio maana aliamua kuondoka Kibaha na kuja Dar es Salaam ili kumuogopa mama yake huyo ambaye alikuwa akimkataza, lakini anasema tangia mama yake alipomuona kwenye televisheni mwenyewe akamruhusu kuendelea na sanaa akiamini siku moja atakuja kunufaika nayo
SOPHIA ABDUL MAARUFU KIBENA KATIKA POZI LA NGUVU

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC