Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kakolanya aitwa Stars, Dida atemwa

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Salum Mayanga amemjumuhisha kipa wa Yanga, Benno Kakolanya katika kikosi chake chenye wachezaji 23 ambacho kitaingia kambini kabla ya kuelekea Misri ambako itaenda kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Lesotho Juni 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Mayanga amemwita Kakolanya ambaye amecheza vizuri katika kikosi cha Yanga hivi karibuni na kuamua kumtema kipa mzoefu Deogratus Munishi "Dida" pia wa Yanga.

Katika orodha ya kikosi hicho cha Stars kitakachoshiriki michuano ya kombe la Cosafa itakayofanyika mwezi ujao nchini Afrika Kusini kimejumuhisha makipa wanne Aishi Manula (Azam FC) na Said Mohamed wa Mtibwa Sugar.

Nyota wengine waliojumuhishwa ni Hassan Kessy, Mwinyi Haji Mngwali (Yanga), Mohamed Hussein "Tshabalala", Abdi Banda (Simba), Salim Abdallah, Agrey Morris, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni (Azam FC).

Wengine ni Himid Mao, Salum Abubakar "Sure Boy (Azam FC), Jonas Mkude, Said Ndemla, Mzamiru Yassin, Shiza Kichuya (Simba) na Simon Msuva (Yanga).

Katika kikosi hicho pia Mayanga amewajumuhisha nyota wa kimataifa ambao ni Thomas Ulimwengu (Eskilstuna ya Sweden), Mbwana Samatta (KRC Genk ya Ubelgiji) na Farid Musa (Tenerife ya Hispania), washambuliaji hao wataungana na mzalendo Mbaraka Yusuf wa Kagera Sugar

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC