Na Paskal Beatus. Dar es Salaam Mshambuliaji wa Simba SC, Ibrahim Ajibu Migomba anawashangaa Singida United kwa kitendo cha kumtangaza kwamba wanataka kumsajili wakati hawajawahi kumwita mezani. Ajibu anashindwa kuwaelewa viongozi wa Singida United timu iliyopanda Ligi Kuu mwaka huu, Akizungumza Mambo Uwanjani, Ajibu amesema mkataba wake na Simba unamalizika mwezi ujao hivyo yuko tayari kusaini kokote. Amedai Singida United inayonolewa na kocha wa zamani wa Yanga, Mholanzi Hans Van der Pluijm imeweka wazi mipango yake ya kumsajili Ajibu lakini bado haijafanya mazungumzo naye hivyo nyota huyo anaweza kuota mbawa
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com