Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Sunche na Kapeto madansa waliotikisa

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Ni miongoni mwa madansa waliojipatia umaarufu mkubwa katika miaka ya 2000 hasa kutokana na aina ya mtindo waliouanzisha.

Sunche na Kapeto (Pichani) ndio ninaowazungumzia leo, nimewamisi sana, ni jamaa zangu wa karibu wote wawili.

Wenyewe wamenigeuza ndugu yao, mara nyingi nimekuwa nao karibu, walianza kucheza kwenye kumbi za starehe na wikiendi hufanya shoo ya nguvu, miaka iliyopita wakati tasnia hiyo ilipokuwa na mashindano yake kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa hadi Taifa, madansa hao ndio walipoibukia.

Walishiriki mashindano hayo kwa kutumia majina ya Big Cut (Kapeto) ambaye ni Kurwa na Small Cut (Sunche) ambaye ni Dotto.

Walifanya vizuri ingawa hawakuwa kuwa mabingwa wa taifa, baadaye waliamua kuachana na majina hayo na kujiita Sunche na Kapeto, walijipatia umaarufu mkubwa.

Baada ya fani ya udansa ilipoanza kudorola, Sunche na Kapeto wakajiunga na Tanzania One Theatle (TOT) iliyokuwa ikiongozwa na marehemu John Komba, TOT Plus Band ilitamba mno hasa ikiwa na waimbaji nyota kama marehemu Ramadhan Masanja "Banzastone", Mhina Panduka na Ally Choki.

Sunche na Kapeto wakaihama TOT na kuamua kujitegemea wenyewe kimuziki, wakaanza kucheza shoo za mitaani, T.I.D akaamua kuwatumis kwenye muziki wake ambapo madansa hao walishiriki kwenye video, ndio wakawa madansa wa kwanza kusheki.

Ama kweli madansa hao wametuachia kitu ambacho kina manufaa kwa muziki wetu, majina yao halisi ni Hassan Abdul (Kapeto) na Hussein Abdul (Sunche) hawa jamaa ni wacheshi na pia ni wapole

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC