Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Makala: Tumuunge mkono Makonda vita ya madawa ya kulevya

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

VITA ya kupambana na madawa ya kulevya imeshaanza na watu mbalimbalj wametajwa kuhusishwa, hatua zimeanza kuchukuliwa na wahusika wameanza kufikishwa mahakamani na wengine bado wanaendelea kuchunguzwa.

Madawa ya kulevya yameua nguvu kazi na kusababisha baadhi yao kuathilika, kwenye upande wa michezo ndio usiseme, vijana wengi wameathiliwa na dawa hizo, kwenye upande wa sanaa pia ni hivyo hivyo, kwa kifupi vijana wanateketea.

Hakukuwa na jitihada zozote za kukabiliana na wafanyabiashara wakubwa wanaoziingiza kutoka Ughaibuni, vilevile hakukuwa na jitihada zozote kuwadhibiti wafanyabiashara wanaosambaza hapa nchini.

Vijana wanazidi kuzitumia na kujikuta wakipoteza nguvu zao ambazo ziljwafanya waweze kujirafutia riziki na baadaye kujikuta hawana nguvu kabisa na kujiingiza kwenye uporaji, makundi ya vijana waliojiingiza kwenye matumizi ya mihadarati wengi wao waporaji.

Na wanafanya hivyo kwakuwa hawana uwezo wa kufanya kazi ambazo ziliwafanya wajipatie pesa, kwa maana hiyo taifa linaangamia, wachezaji nao wakawa wanaathiliwa na dawa hizo na kujikuta wakipoteza viwango vyao.

Tumeshuhudia wachezaji kadhaa hapa nchini wakijihusisha moja kwa moja na matumizi ya madawa ya kulevya na pia wakapoteza viwango vyao, sipo hapa kutaja majina ya wachezaji hao lakini wengi wao wanafahamika lakini siwezi kumtaja mmoja mmoja.

Madawa ya kulevya ni pamoja na "Unga", Bangi na Mirungi, Unga umegawanywa makundi mbalimbali kulingana na thamani yake, kuna Cocaine, Heroin na nyinginezo, lakini Bangi na Mirungi ni aina moja tu ya majani ambayo yanatajwa kuwa ni hatari kwa afya ya mtumiaji.

Wasanii nao wengi wao wamepoteza vipaji vyao kutokana na kutumia dawa hizo, na kwa bahati mbaya wengineo walipoteza maisha, msanii Langa aliyetamba na kundi la Wakilisha lililokuwa na wasanii watatu, yeye, Sarah na Witness, alifariki dunia na kifo chake kilitajwa kuwa kimetokana na matumizi ya dawa za kulevya.

Ukiachana na Langa, msanii mwingine aliyefariki kwa dawa za kulevya ni Mangwea, msanii huyo alifia nchini Afrika Kusini na inasemekana kabla ya kuanza safari alitumia dawa hizo, na zipo baadhi ya Clip za video zilizoonyesha madaktari wa nchini Afrika Kusini wakiufanyia upasuaji mwili wa msanii huyo uliokuwa na dawa nyingi za kulevya ambazo alizimeza ilj azilete Tanzania.

Wasanii wanatajwa kubeba dawa za kulevya na wapo waliokamatwa ndani na nje ya nchi, pia wapo wasanii wanaotumia dawa hizo, Ray C mmoja wa wasanii waliotikisa kwenye muziki lakini akapoteza kipaji chake kwa kutumia dawa hizo, kwa sasa Ray C si yule wa miaka ile.

Daz Baba ambaye naye alitamba kwenye kundi la Daz Nundaz lililotikisa naye ameangamia kwa dawa za kulevya, Daz kwa sasa ni muathilika wa dawa hizo, ukiachana na Daz, Chid Benz rapa aliyeibuka kwa kasi ya ajabu akiwa na sauti nene naye ameangamia kwa dawa hizo.

Chid Benz aliyetamba na wimbo wa Darisalaam Stand Up, kwa sasa ni muathilika wa dawa hizo, T.I.D naye alijiingiza kwenye matumizi hayo na kujikuta anapoteza sauti yake tamu aliyotamba nayo kwenye wimbo wa Zeze, wasanii wetu wanaangamia.

Lakini inasemekana kuwa wasanii hao hao wamekuwa wakishiriki kusambaza dawa hizo kwa wenzao, wasanii wanaotajwa kuwauzia wenzao ni Dogo Hamidu, Mr Blue, Wema Sepetu na wengineo ambao wamejumlishwa kwenye majina 65 yaliyotangazwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Poul Makonda.

Makonda ameamua kupambana na madawa ya kulevya na tayari watu kadhaa wameshahojiwa na Jeshi la Polisi, Makonda hakusita kuwataja wafanyabiashara wakubwa wanaodili na dawa hizo mpaka kuleta tafrani kwa wananchi ambao wameanza kumshutumu.

Makonda ametaja majina makubwa ambayo ndani yao wamo viongozi wa kisiasa, dini na soka, lakini nguvu inapaswa kuongezeka kwa Makonda ili kumuunga mkono kwenye sakata hili, asibaki peke yake kwani tumeshapoteza wasanii wengi na wanamichezo ambao wangetuletea sifa kubwa kwenye taifa letu.

Lakini pia vijana wengi wameangamia kwa dawa za kulevya na kujikuta wakijiingiza kwenye uharifu mwingine kama wa uporaji, maisha yetu huko mtaani yamekuwa ya shida, kama umevaa vito vya thamani ujue uko shakani kwani "Mateja" wakikuona kwao ni furaha.

Wanaamini wakikubana watapata hela ya kununulia 'Unga', nimeshawahi kumuona "Teja" akishiriki kujiibia yeye mwenyewe ili akapate unga japo kidogo kwani alikuwa alosto kama wenyewe wanavyoita, mteja huyo aling' oa mabati ya nyumba yake ya urithi na kwenda kuuza

Tuungane na Makonda kwenye vita hii na tuache ushabiki kwa wale wanaotajwa, tusiwaamini sana watu waliojichomeka kwenye siasa, michezo na dini, inawezekana waliotajwa ni walengwa tosha ila kelele za kuwatetea ni nyingi mno

ALAMSIKI

Msanii T.I.D ni mmoja wa waathilika wa dawa za kulevya
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Poul Makonda (Kulia) akiteta na Waziri wa Habari, Michezo, Utamaduni na Wasanii Mhe Nape Nnauye

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC