Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Makala: Chakori ni funzo kwa wasanii wetu, wabadilike

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Wasanii Mhe Nape Moses Nnauye majuzi alipiga marufuku uingizwaji na usambazwaji wa filamu za kigeni kwa vile zinaua soko la filamu za ndani.

Hii yote imetokea baada ya filamu za Kitanzania maarufu Bongomovie kukosa soko, Wapenzi wa filamu nchini hawanunui tena filamu za hapa na wamekuwa wakitazama filamu za kigeni.

Kwa maana hiyo wasanii wetu nchini wanakosa pesa za kuendesha maisha yao na kujikuta wakijitumbukiza kwenye skendo, hakuna mtu anayemfuatilia JB, Ray au Wema Sepetu, wala hakuna mtu anayemfuafilia Jengua, Irene Uwoya wala Johari, kwa kifupi wasanii wetu wamepoteza mvuto wa kibiashara tangu alipotutoka Steven Kanumba.

Waziri Nape mbali ya kuzipiga stop filamu za nje, pia aliwataka wale wafanyabiashara wa maeneo ya Kariakoo hasa mitaa ya Agrey, Kongo na Msimbazi ambako ndiko inakofanyika biashara ya usambazaji wa filamu hizo kuacha mara moja mpaka pale utaratibu utakapopangwa.

Inasemekana filamu za nje hazilipi kodi, nyingi zimekuwa zikipatikana kwa njia ya Kudownload kupitia mitandao, hali ya soko la filamu zetu limezidi kushuka, wasanii wanalia kila kukicha kuwa maisha magumu, yaani hawauzi, na Mhe Nape amesikia kilio chao na kuamua kuziondoa sokoni muvi za nje.

Filamu za Kinigeria, Amerika, Uchina na Uhindi zimekuwa zikifanya vizuri sokoni na kuliangamiza kabjsa soko la filamu za ndani, watu hawana mpango tena na JB, watu hawataki kumsikia tena Wema Sepetu na ndio maana wasanii wetu wamekuwa wakifanya biashara haramu kwakuwa biashara halali hailipi, Wema ukitaka kumuona nenda Central ana kesi ya madawa inamsumbua.

KIPI KIMEWAANGUSHA?

Ukiangalia kwa haraka unaweza kusema kilichowaangusha ni anguko la uchumi hapa nchini mwetu na watu kukosa pesa za kununua kazi zao, siyo siri bei ya filamu zetu ziko juu kuliko zile za kigeni, hivyo watu wengi wameamua kununua filamu za kigeni.

Lakini kiundani kabisa kilichowaangusha wasanii wetu ni kuiga tamaduni za Kimagharibi, wengi wamechoshwa na mambo ya kuiga wazungu, Wasanii wetu badala ya kuutangaza utamaduni wa Kitanzania wamejikuta wakitangaza tamaduni za Kizungu.

Hapo wamejikuta wakipotosha jamii badala ya kuielimisha, wasanii wetu wamejikuta wakiiharibu jamii ya Kitanzania, watoto wetu wanaiga kupitia filamu hizo hizo ambapo nao wamekuwa wakivaa kama akina Wema Sepetu au Irene Uwoya, wasichana ndio wameharibika kabisa maana wanatembea uchi barabarani.

Ni aibu hata kuongozana nao maana utadhalilika, vijana wa kiume nao wamekuwa wakivaa mlegezo jambo ambalo ni hatari kwao, hizo ndio filamu zetu za ndani ambazo Mhe Nape ameamua kuzitetea, kiukweli Nape alipaswa kuwaambia ukweli tu kuwa kazi zetu hazifai na wajikite kwenye uhalisia wa tamaduni zetu.

Nimekuwa mpenzi mkubwa wa kutazama filamu za kigeni hasa ya Kihindi, na sasa nafuatilia vema 'Season' ya Udaan ambapo ndani yake yupo Chakor ambaye anaibeba Season hiyo, kwakweli Mhe Nape naye alipaswa kuitazama season hiyo kisha angewaambia ukweli wasanii wetu waige kitu kutoka kwenye season hiyo badala ya kuifungia.

Season hiyo inafundisha, inaelimisha na inaburudisha, pia sijaona sehemu inayopotosha jamii, hizo ndio kazi nzuri ambazo zilipaswa kufanywa na wasanii wetu ambao wamejikuta wakishiriki kuharibu kizazi chetu, season ya Udaan inapendwa hata na watoto wadogo kwani imekuwa rafiki na watu wote.

Nasikia na hiyo nayo imezuiwa na Nape, namuomba Mheshimiwa Nape awaambie ukweli wasanji wetu kuwa Watanzania hasa watazamaji wa filamu tunataka tamaduni zetu zionekane kama ilivyo kwa wenzetu wa India ambao wamekuwa wakituonyesha tamaduni zao, Mwisho namalizia kwa kusema Hili filamu za Kibongo zitawale soko zinahitaji akili na maarifa ya ziada ama sivyo tutazipiga kumbo kabisa

Chakor mmoja kati ya washiriki wa Season hiyo yenye mafunzo
Chakor akiwa kwenye pingu nzito ya mateso ya utumwa

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC