Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: SIMBA ITAJUTIA MAAMUZI YAKE

Na Prince Hoza

Simba SC inaelekea kubaya, nina maana viongozi wake wanakurupuka kwa kutoa maamuzi yasiyo na tija kwa mashabiki wake, Simba kwa sasa inakamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Timu hiyo ilikuwa ikiongoza ligi hiyo kwa kipindi kirefu lakini jana iliondolewa rasmi kileleni hasa baada ya jana Yanga SC kushinda mabao 2-0 dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Yanga waaongoza kwakuwa na pointi 46 wakati Simba iliyofungwa bao 1-0 na Azam juzi Jumamosi katika uwanja huo huo wa Taifa ina pointi 45, tatizo linaloonekana kuiathili Simba ni kukosekana kwa muunganiko wa pamoja wa wachezaji wake.

Benchi la ufundi linaloongozwa na Mcameroon Joseph Omog libaonekana kushindwa kufanya kazi yake ipasavyo, lakini mimi wala simlaumu hata kidogo Omog kwani karibu wachezaji wote walioko Simba hakuhusika katika usajili wao.

Wachezaji wa Simba walisajiliwa kwa matakwa ya viongozi na wanachama wao na ushabiki ulihusika zaidi, Omog alisajiliwa wachezaji na akapewa akaambiwa ni wazuri na ubingwa ni ajenda yao msimu huu.

Kamati ya usajili ya Klabu hiyo inayoongozwa na mwenyekiti wake Kapteni mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Zacharia Hanspope akawatangazia Wanasimba kuwa straika Hamisi Kiiza raia wa Uganda hafai mnafiki hasa baada ya msimu uliopita kuanzisha mgomo baridi wa wachezaji wa kigeni.

Kiiza aliwaongoza wachezaji wenzake wa kigeni kugomea ili walipwe pesa zao za mishahara, mgomo huo uliungwa mkono na Jjuuko Murushid, Brian Majwega, Poul Kiongera, Vincent Angban na Justuce Majabvi, na baadaye nyota hao wakaachwa na wawili tu ndio walionusurika ambao ni Jjuuko na Angban aliyeachwa msimu huu.

Kiiza ambaye aliibuka mfungaji bora kwenye kikosi cha Simba akifanikiwa kufunga mabao 19 akishika nafasi ya pili nyuma ya Amissi Tambwe aliyeibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Tambwe alifunga magoli 21 na kutwaa kiatu cha dhahabu.

Kilichonishangaza kwa viongozi wa Simba kwamba wameamua kumuacha Kiiza kwa madai eti ni mtovu wa nidhamu kwa sababu amewadai oesa zake za mshahara, kwani kudai haki yako ni kosa? Viongozi wa Simba wametudanganya kwa kusema Kiiza hafai na wamsajili straika Laudit Mavugo kutoka Burundi.

Mpaka sasa Mavugo amefunga magoli matano tu, hii ni mara ya pilj kwa Simba kuachana na wafungaji wake wazuri, iliwahi kumtema Amissi Tambwe aliyeibuka mfungaji bora kwa kufunga magoli 19 na msimu uliofuata akatua zake Yanga ambapo yupo hadi sasa.

Kwakweli Simba watajutia sana maamuzi yao ambayo yanawagharimu, nina imani kama angekuwepo Kiiza huenda tungeshuhudia Simba ya mwendokasi ambayo ingekuwa suluhisho kwa mashabiki wake.

Ila bado sijawakatia tamaa wanaweza kutwaa ubingwa kama watayafanyia kazi mapungufu yaliyopo, tatizo ambalo naliona pale ni kukosekana kwa mshambuljaji namba moja ambaye yeye kazi yake ni kucheka na nyavu, Mavugo na wengine waliopo Simba ni washambuliaji namba mbilj kwa mfano Ibrahim Ajibu, Mohamed Ibrahim na Juma Luizio

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC