Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Staa Wetu: Mshamu Hassan "Mfuga Njiwa" Mtangazaji chipukizi wa mpira wa miguu, mwenye ndoto za kumfikia Juma Nkamia

Na Prince Hoza, Dar es Salaam

Anaitwa Mshamu Hassan lakini anajulikana zajdi kwa jina la Baba Nuraty Mfuga Njiwa, Ni mtangazaji wa redio Sibuka 94.5 FM inayosikika nchi nzima ikiwemo Dar es Salaam.

Mtangazaji huyo ameanza kujipatia umaarufu mkubwa kutokana na utangazaji wake kuvutia wengi na wale waliopata bahati ya kumsikia wamefurahishwa naye.

Alianza kazi hiyo akiwa kama mwanasalamu wa kawaida katika redio mbalimbali kiasi kwamba akajipatia umaarufu, Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu, Mfuga Njiwa alisema utangazaji ni kazi aliyoipenda ingawa hakupata kujua ataianzia wapi.

Salamu zilimwezesha kupata nafasi ya kujulikana na wengj na ndipo alipoweza kufanya interview katika vituo vya redio 13 na kimoja cha televisheni, Lakini anasema ni redio Sibuka pekee ndiyo iliyotambua kipaji chake.

Akaanza kazi katika redio hiyo na kipindi cha michezo cha kila siku cha Sportaiment na kile cha wiki kinachofanyika kila siku ya Jumamosi kiitwacho MBS ambavyo vyote anashiriki.

Pia Mfuga Njiwa amekuwa akipata nafasi ya kutangaza mpira wa miguu, Mtangazaji huyo ameanza kusikika katika mechi kadhaa za kirafiki na zile za Ligi kuu bara zinazofanyika katika viwanja mbalimbali hapa nchini.

Mfuga Njiwa aliyepata elimu yake ya msingi na sekondari Temeke Dar es Salaam  alizaliwa katika hospitali ya Temeke mwaka 1983, baba yake ni mzaliwa wa Mikindani mkoani Mtwara wakati mama yake ni mzaliwa wa Kilwa mkoani Lindi.

Mtangazaji huyo chipukizi ana ndoto kubwa za kumfikia mtangazaji mkongwe Juma Nkamia ambaye kwa sasa ni mbunge, Nkamia alikuwa akitangaza vema mpira wa miguu alipokuwa katika redio ya TBC Taifa.

Kwa wale waliobahatika kumsikia wanakiri kabjsa kuwa Mfuga Njiwa ni Nkamia wa pilj kwani ana kasi kubwa anapotangaza na akionekana kama mzoefu, aidha mtangazaji huyo huwa sambamba na wenzake David Pasko, John Ndeki, Salama Ngale, Omary Juma na mwingine anayefahamika kwa jina la Promise

Mfuga Njiwa akiwa kazini
Akiwa studio akifanya yake

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...