Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: MATTEO ANTONY SIMON, MKOMBOZI WA YANGA ALIYEIBEBA KIMATAIFA

Na Prince Hoza, DAR ES SALAAM

WENGI wanajua mashujaa wa Yanga ni Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Thabani Kamusoko, Lakini wanashindwa kufahamu kwamba Yanga SC inaye shujaa ambaye si mwingine ni Matteo Antony Simon.

Huyo ni mshambuliaji wa Yanga ambaye alisajiliwa mwanzoni mwa msimu uliopita akitokea KMKM ya Zanzibar, Matteo ilikuwa asajiliwe na Simba lakini kama unavyofahamu vigogo hao wa soka nchini wamekuwa na kawaida ya kunyang' anyana wachezaji.

Hatimaye Matteo akatua Yanga ingawa hakuwashangaza mashabiki wa timu kwakuwa hakuwa maarufu, mshambuliaji huyo aliyeonekana msumbufu tangia akiwa na kikosi cha KMKM, hakuwa katika kikosi cha kwanza cha Yanga kinachonolewa na Mholanzi Hans Van der Pluijm.

Matteo alikuwa akianzia benchi na hii yote inatokana na Yanga kuwa washambuliaji wengi ambao wamekuwa msaada mkubwa kwenye klabu hiyo ambayo msimu uliopita iliweza kukusanya vikombe vyote vikubwa hapa nchini.

Yanga imeweza kuchukua Ngao ya Hisani ikiwafunga Azam FC kwa mikwaju ya penalti 8-7, pia imetwaa ubingwa wa ligi kuu bara pamoja na kombe la FA, Yanga imetinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika.

Kabla haijaingia hatua hiyo, Yanga ilianza kucheza michuano hiyo kuanzia raundi ya awali, Yanga ilianzia michuano ya Ligi ya mabingwa barani Afrika ambapo iliwatoa Cerce de Joachim ya Mauritius.

Baadaye ikaifungasha virago APR ya Rwanda, kisha Yanga ikaondoshwa na Al Ahly ya Misri ambapo ikaangukia kombe la Shirikisho barani Afrika, hapo ndipo ilipojikuta inakutana na Sagrada Esparanca ya Angola.

Mchezo wa kwanza ulipigwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam ambapo Yanga ilishinda kwa mabao 2-0, alikuwa Simon Msuva ndiye aliyepeleka furaha Jangwani kwa bao lake tamu la kuongoza.

Yanga ilipata bao hilo kunako kipindi cha pili na siku hiyo ilionekana kukosa mabo na hasa kukosekana kwa mshambuliaji wake tegemeo Mzimbabwe Donald Ngoma, kipindi cha pili Yanga walianza kusherehekea mabao, Matteo Antony Simon alipiga shuti kali la umbali wa mita 40 ambalo lilikwenda moja kwa moja wavuni.

Kwa maana hiyo Yanga iliwatoa Sagrada kwa jumla ya mabao 2-1 kwani katika mchezo wa marudiano uliofanyika Angola Yanga ililala 1-0 lakini goli la Matteo halikuweza kusawazishwa hivyo nyota huyo Mzanzibar anakuwa shujaa wa Yanga na ndiye aliyeivusha Yanga kimataifa



Matteo Simon Antony mwenye rasta akishangilia bao lake muhimu lililoivusha Yanga

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC