Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONI: TFF WAMESAHAU MAJUKUMU YAO

Na Prince Hoza, DAR ES SALAAM

KAZI kubwa inayotakiwa kufanywa na Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF kuendeleza soka hapa nchini, pia kazi yao nyingine ni kuhakikisha maadili yanakuwepo kwenye mchezo huo.

Maadili yenyewe ni usimamizi bora, na haki kwa mashindano yote wanayosimamia, kwa bahati mbaya TFF ya sasa inaongozwa na rais wake Jamal Malinzi imeshibdwa kusimamia vyote hivyo.

Malinzi ameshindwa kufuata nyayo za mtangulizi wake Leodegar Chila Tenga ambaye ameondoka TFF lakini bado anakumbukwa kutokana na mema yake aliyoyafanya.

Malinzi ameshindwa kusimamia maadili ambapo inafikia watu wa ngazi ya chini wanashindwa kuwaheshimu viongozi wao, kwa mfano soka la Tanzania mwaka huu limegubikwa na kashfa ya rushwa ambapo Shirikisho hilo nalo limetajwa kuhusika.

Likiwa tayari limeshawapa baadhi ya watu adhabu kubwa ikiwemo kuwafungia maisha makocha na viongozi wa timu, pia wapo baadhi ya wachezaji nao wameadhibiwa.

Hii yote imetokana na uuzo uliopo ndani ya Shirikisho hilo la kandanda hapa nchini, wakati TFF ikishindwa kusimamia vema masuala yake, imejikuta ikilumbana na wasemajj wa vilabu.

Hivi karibuni msemaji wa klabu ya Yanga alilijia juu Shirikisho hilo na hasa kutokana na kitendo chao cha kukaa na zawadi yao kama mabingwa wa kombe la FA, Yanga walipaswa kukabidhiwa kitita chao cha shilingi Milioni 50.

Lakini hadi sasa bado hawajalipwa, kitendo hicho kimemfanya msemaji wa Yanga Jerry Muro kulalamika, TFF wamemtia hatiani Muro wakidai anawachafua wakati ni ukweli .mtupu aliosema.

Pia Muro amenanga tena TFF kwa kitendo chao cha kukalia vifaa vyao vya michezo walivyokabidhiwa na Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF, Yanga ilipaswa kupewa vifaa hivyo kabla hata haijacheza mechi yake ya kwanza dhidi ya MO Bejaia ya Algeria.

Lakini Shirikisho hilo likakalia vifaa hivyo mpaka ilipowakabidhi kwa mbinde tena ikijiandaa kucheza na TP Mazembe Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, kwakweli TFF hii ya Malinzi imechoka wacha tuseme ukweli.

Malinzi na watu wake pale TFF wameshindwa kuiwezesha Taifa Stars kufuzu mashindano yoyote yale, kila tunapofikia kushiriki kombe la Dunia, Mataifa Afrika na kombe la Chan Tanzania tumekuwa wasindikizaji.

Kwa kifupi hatuna timu ya taifayenye spidi kama ile ya mtangulizi wake Tenga ambayo kidogo ilifanikiwa kututoa kimasomaso kwa kufuzu fainali za Chan mwaka 2008, Malinzi ameona ni bora kuiingiza TFF kwenye migogoro na vilabu.

Leo hii amemfungia Muro kwa kosa la kuwaambia ukweli kesho atakuja kuifungia Yanga au Simba kama itadai zawadi yake ya ubingwa wa bara kwani tayari wameonyesha udhaifu mkubwa kwa kushindwa kuwapa Yanga zawadi yao ya  ubingwa wa kombe la FA

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC