Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ANAYEKUMBUKWA: HABIBU MAHADHI, MFUNGAJI BORA LIGI KUU SAFARI LAGER 1998

Na Salum Fikiri Jr, DAR ES SALAAM

ANATOKEA kwenye familia ya marehemu Omary Mahadhi bin Jabir kipa wa zamani wa African Sports, Simba SC na Taifa Stars, Habibu Mahadhi ni mtoto wa gwiji hilo la soka miaka ya 70 na 80.

Habibu alitamba na Coastal Union ya Tanga akitumia guu la kushoto na aliibuka mfungaji bora wa Ligi kuu ya Safari Lager mwaka 1998 wakati huo ikichezwa kwa hatua ya makundi.

Habibu aliyeanzia kwenye timu ya mtaani kwao Magomeni Kota ya Police Kids baadaye akajiunga na Big Bon ya Magomeni Mikumi timu aliyokaa nayo hadi aliporejea timu ya mtaani kwake ya Messina Linea.

Big Bon iliyoanzia Ligi Daraja la nne ikapanda hadi Daraja la Tatu ngazi ya mkoa wa Dar es Salaam, kwa bahati mbaya timu hiyo ikavunjwa hasa baada ya aliyekuwa mfadhili wake Ahmed Bashwani kuachana na ufadhili.

Mahadhi na wenzake wakaondoka na ndipo alipojiunga na Messina, Mahadhi na nyota mwenzake George Kavila wakaenda zao Coastal Union ya Tanga na katika msimu wake wa kwanza akaibuka mfungaji bora wa ligi kuu bara.

Chakushangaza mchezaji huyo ambaye ni kaka wa Waziri Mahadhi "Mendieta" aliyepata kutamba pia na Coastal Union, Yanga na Moro Ubited pamoja na Taifa Stars alizikacha ofa za Yanga na Simba.

Mahadhi akitumia guu lake la kushoto alikataa ofa ya Yanga kisha baadaye ya Simba na kikubwa alisema timu hizo zingekuwa tayari kumpa dau kubwa angejiunga na moja wapo, Mahadhi alilamba Milioni moja ya ufungaji bora ambayo ilimsaidia kukamilisha ujenzi wa nyumba yake maeneo ya Mbezi jijini Dar es Salaam

Habibu Omari Mahadhi akiwa amejipumzisha nje ya nyumba yake

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC