Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONI: SIMBA WEKENI MAMBO HADHARANI, USAJILI WA KIMYA KIMYA MAANA YAKE NINI

Na Prince Hoza, DAR ES SALAAM

NIMEMSIKIA mwenyewe mwenyekiti wa kamati ya usajili klabu ya Simba Kapteni mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Zacharia Hanspoppe akisema kwamba Simba itafanya usajili wake kimya kimya.

Maneno hayo si kwamba yamenikera mimi peke yangu hapana, wapo mashabiki wa Simba wameniandikia meseji kwamba hawafurahishwi na Hanspoppe  mashabiki hao wanataka bosi huyo wa usajili ajiweke kando ili awapishe wengine.

Usajili wa kimya kwa sasa hauna maana yoyote ikiwa mchezo wa mpira unachezwa hadharani, hakuna faida yoyote ya kufanya usajili kwa kuogopa wenzako wanafanya nini.

Hivyo namuomba Hanspoppe aachane na maneno hayo na awasajilie majembe Wanasimba ili wasuuzike na mioyo yao, Tetesi za usajili zimeanza kuenea kuwa Sinba wamemsajili kiungo wa Yanga Salum Telela.

Mbali na Telela pia Simba inatajwa kukamilisha dili ya kumchukua mshambuliaji wa Ndanda FC ya Mtwara Atupele Green, Hanspoppe kutuambia usajili utakuwa wa kimya kimya anamaanisha nini! Paul Kiongera (Pichani) amesajiliwa na Simba akitokea KCB ya Kenya lakini hatuzioni cheche zake.

Mshambuliaji huyo alisajiliwa mwishoni mwa kufungwa kwa dirisha la usajili, kusajili kimya kimya hakuna faida ikiwa Yanga wanawasajili wachezaji wote wanaoaminika kuwa ni wazuri, Yanga tayari wamewasajili Hassan Kessy, Benno Kakolanya, Vincent Andrew "Dante" na wengineo.

Usajili huo umeonekana kuwashtua Simba kwani tayari baadhi ya wachezaji waliosajili Yanga walikuwa wakipigiwa hesabu za kutua Simba, Lakini ukimya wa viongozi wa Simba ukasababisha nyota hao kusainishwa Yanga.

Wakati dirisha la usajili likitazaniwa kufunguliwa kesho kutwa, mabosi wa kamati ya usajili wanasema hadharani kwamba watasajili kimya kimya, ina maana mambo yao hayatakuwa hewani.

Huo sasa ni usajili wa magumashi maana mashabiki hawataweza kujua hatma ya timu yao msimu ujao, Lakini kuna fununu nyingi tu ambazo mashabiki walitakiwa kuzifahamu mapema.

Usajili wa kimya kimya una faida na hasara, faida yake ni kumsajili mchezaji mzuri ambapo wapinzani wako hawamjui, Mambo ya fedha nayo yanahusika katika zoezi hili la usajili.

Kwa mfano Simba inataka kumchukua Salum Telela halafu wanataka kumpa milioni 20 lakini Azam au Mwadui wakampandia dau na kumalizana nao, Hanspoppe anatakiwa kuweka mambo hadharani ili Wanasimba wafurahie timu yao

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC