KOCHA MPYA SIMBA ATUA KUSAINI MKATABA

Na Prince Hoza

KOCHA mpya wa klabu ya Simba Mcameroon Joseph Maurus Omog anatarajia kuwasili Alhamisi tayari kabisa kusaini mkataba wa kuinoa timu hiyo msimu ujao.

Omog ambaye aliwahi kuzinoa Leopards ya DRC na Azam FC ya Tanzania zote akiziwezesha kupata ubingwa wa nchi, anataraji kuiongoza Simba kwa ajili ya msimu ujao na huenda akasaini mkataba wa miaka miwili.

Habari ambazo Mambo Uwanjani inazo zinasema kuwa Omog atakuwa kocha mkuu ndiye atakayependekeza usajili wa wachezaji wa kimataifa, Omog alizaliwa Novemba 30, 1971 Cameroon na amekuwa kocha nwenye mafanikio.

Msimu ujao Simba ishindwe yenyewe kutwaa ubingwa wa bara kutokana na bahati aliyokuwa nayo na uwezo pia, kikosi cha Simba kinasukwa upya huku Jackson Mayanja akitajwa kuwa msaidizi wake

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI