Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: DEOGRATUS MUNISHI 'DIDA', SHUJAA WA YANGA NA TANZANIA KWA UJUMLA

Na Exipedito Mataruma, DAR ES SALAAM

MACHO yake yalikuwa makini kuitazana penalti iliyopigwa dakika ya 87 zikisalia dakika tatu mpira kumalizika, si mwingine ni Deogratus Boniventure Munishi maarufu kama Dida akifananishwa na kipa wa Brazil Nelson Dida.

Dida alikuwa shujaa Jumatano iliyopita ikifanikiwa kuiondosha mashindanoni GD Sagrada Esperanca ya Angola kwa jumla ya mabao 2-1, Yanga ilishinda magoli 2-0 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam shukrani kwa Simon Msuva na Matheo Antony waliofunga mabao safi kabisa.

Yanga ilifungwa bao 1-0 katika Uwanja wa Esparanca mjini Dundo Angola goli lililofungwa na mkongwe Love Caburunca, matokeo hayo yameivusha Yanga hadi hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika ikiwa ni historia katika ukanda wa Afrika mashariki.

Yanga inakuwa timu ya kwanza ya nchini kufikia hatua hiyo, pia ikumbukwe Yanga iliwahi kufanya hivyo mwaka 1998 ilipotinga makundi ligi ya mabingwa barani Afrika.

ALIFIKAJE YANGA!

Dida alianza kuchomoza akiwa na Manyema ya Ilala ambako ndiko kulikochangia mafanikio yake, Dida alichagua nafasi ya kipa badala ya nafasi nyingine za uwanjani hasa kutokana na urefu alionao ulimfanya haweze kucheza mipira ya juu.

Dida alifanya vizuri na Manyema mpaka uongozi wa Simba ukaamua kumchukua, Dida na Bakari Kigodeko ndio wachezaji pekee wa Manyema waliosajiliwa na Simba, kipa huyo alisajiliwa Simba hasa baada ya kuachana na kipa wake Amani Simba.

Kipa huyo alikutana na makipa wazoefu Juma Kaseja na Ali Mustafa 'Barthez' ambao hata hivyo hakuwaogopa, Dida alijiunga na Simba mwaka 2008 na mechi yake ya kwanza ilikuwa dhidi ya Villa Squad Simba ikishinda 4-1 na uliofuata dhidi ya Polisi Dodoma ukiisha kwa sare ya 2-2.

Anasema alipata unafuu wa kupata namba Simba hasa baada ya Juma Kaseja kuhamia Yanga, Dida aliyezaliwa mwaka 1989 Moshi, Mkoani Kilimanjaro katika familia ya mzee Boniventure Munishi na mama Hilda Temu akiwa ni mtoto wa pili katika familia hiyo ya watoto wanne, nduguze ni Ismail, Kasija na George.

Alisoma Madenge shule ya msingi kuanzia mwaka 1996 mpaka 2002 kisha kujiunga na Makongo Sekondari mwaka uliofuatia lakini alisoma kwa mwezi mmoja tu na kujikita katika soka, alianza kucheza soka mwaka 1993 katika viwanja vya Temeke msikiti wa Tungi.

Dida alijiunga na timu ya Temeke Kids nwaka 2000 iliyokuwa chinj ya kocha Tunge na kufanya mazoezi katika viwanja vilivyokuwepo jirani ya uwanja wa Taifa wa zamani (Sehemu hiyo sasa uwanja mkuu wa Taifa).

Mwaka 2004 alisajiliwa na Coastal Union ya Tanga na kucheza Ligi Daraja la kwanza, mwaka uliofuata alijiunga na timu ya Chuoni ya Zanzibar iliyokuwa inashiriki ligi Daraja la kwanza visiwanj humo.

Mwaka uliofuata alijiengua na kurudi Dar es Salaam na kuendelea kujifua katika viwanja vya Tungi Temeke, Februali 2007 alijiunga na Makondeko ya Temeke lakini Machi mwaka huo huo alijiunga na Mkunguni ya Ilaka kushiriki ligi Daraja la tatu.

Hapo hakukaa sana kwanj Aprili 2007 alijiunga na Manyema na kufanikiwa kuipandisha ligi kuu bara, Manyema ndiyo timu iliyomfungulia milango Dida kuzichezea klabu kubwa nchini za Simba Sc, Mtibwa Sugar, Azam Fc na sasa Yanga Sc pia akiitwa Taifa Stars.

Dida ameweza kuipa ubingwa wa bara Yanga mara mbili mfululizo huku pia akifanikiwa kuiwezesha kuingia fainali kombe la Azam Sports Federation Cup maarufu FA Cup ambapo Jumatano ijayo watacheza fainali na Azam Fc.

Deo Munishi akionyesha umahiri wake wa kudaka mashuti
Dida alipobebwa juu juu na mashabiki wa Yanga hasa baada ya kuwa shujaa

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC