Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BMT, TFF MNATAKA KUIPELEKA WAPI YANGA?

Na Prince Hoza, DAR ES SALAAM

BARAZA la Michezo la Taifa (BMT) lilipokea agizo kutoka Wizara ya Habari, Michezo, Utamaduni na Wasanii la kutaka vyama vyote vya michezo na vilabu ambavyo havijafanya uchaguzi vifanye haraka ifikapo Juni mwaka huu.

Waziri wa wizara hiyo Nape Moses Nnauye alikuwa mstari wa mbele kuvitaka vilabu na vyama kuchaguana kwa njia ya kidemokraisa, BMT ililigeukia Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF na kulitaka liwaambie wanachama wao ambao hawajafanya uchaguzi wafanye haraka mwaka huu.

Yanga SC ikakutwa na hatia kwani haijafanya uchaguzi wake kisheria tangu mwaka 2014 ambapo muda wa uongozi wao ulifikia tamati, hata hivyo wanachama wa klabu hiyo walimuongezea muda zaidi nwenyekiti wao Yusuf Mehbood Manji kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Manji aliendelea kukaa madarakani kwa mwaka mmoja zaidi na makubaliano yao wafanye uchaguzi mwaka jana 2015, lakini nao pia hawakufanya tena uchaguzi na kisingizio kikubwa ni uchaguzi mkuu wa nchi ambao ulifanyika Oktoba 25, 2015.

Safari hii sasa TFF imeikomalia Yanga kufanya uchaguzi huo lakini kwa masharti magumu mno, TFF imeanzisha mchakato huo kwa kuwataka Wanayanga kuchukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali kwenye Shirikisho hilo.

Kamati ya uchaguzi huo ni ya TFF ikishirikiana na sekretalieti ya Yanga kwa ajili ya kuwatambua Wanayanga, lakini Kamati hiyo ya TFF inataka kutumia katiba Yanga ya mwaka 2010 huku pia ikiwazuia wanachama wa Yanga wenye kadi mpya za ATM hawataruhusiwa kupiga kura.

Yanga wanayo kamati yao ya uchaguzi inayoongozwa na Sam Mapande ambayo pia ikisimamia mchakato huo, kitendo cha Yanga kunyimwa haki ya kusimamia uchaguzi huo kungepelekea utaratibu wa kufanyika uchaguzi huo.

Yanga wangehitisha mkutano mkuu wa wanachama na wangeamua wenyewe watumie katiba ipi, kuna uwezekano mkubwa baadhi ya Wanayanga wenye mapenzi na klabu yao, pia kuna athali Yanga wakapata viongozi wasiokuwa na mapenzj na timu yao.

Miaka ya nyuma Yanga walikuwa na viongozi wao ambao kila kukicha mwenendo wa timu yao haukuwa mzuri, mitaa ya Jangwani na Twiga bakora zilitapakaa mpaka FFU walitumika kutuliza ghasia, Lakini kwa sasa Yanga wanafurahia timu yao kiasi kwamba hata mahasimu wao Simba wanaona donge.

Yanga ikiwa chini ya mwenyekiti wake Bilionea Yusuf Mehbood Manji imefanya mambo mengj ya maana ikiwemo kuhudumia wachezaji wake vizuri, Yanga imetwaa ubingwa wa bara mara mbili mfululizo, Ngao ya Jamii mara mbili mfululizo na kombe la FA, pia Yanga imetinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika.

Yanga hiyo hiyo imeweza kumtambia mtani wake Simba Sc kwa kumfunga mara mbili mfululizo, Yanga iliifunga Simba mabao 2-0 kila mechi za Ligi kuu bara.

Wakati Yanga ikiwa inafanya vizuri lakini viongozi wake sidhani kama wana kadi za zamani kama inavyotaka TFF, kwa maana hiyo kuna uwezekano mkubwa Yanga ikapotea kwa staili hiyo, TFF wanaweza kuifanya Yanga iongozwe na mamluki ambao watatumia mwanya huo.

Sifurahishwi na uchaguzi wa Yanga unaosimamiwa na TFF, inafahamika waziwazi kwamba Yanga inajiendesha yenyewe hivyo inapaswa kuamua hatma yake yenyewe, mimi si mwanachama wala mpenzi wa Yanga lakini siungi mkono unafiki huu wa TFF na BMT ambao wanataka kuipeleka Yanga huko kusikojulikana

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba 0652626627

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC