Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA WATAKIWA KUFANYA UCHAGUZI JUNI 5

Na Mwandishi Wetu  DAR EA SALAAM

SHIRIKISHO la soka nchini TFF limeitaka klabu ya Yanga kuitisha uchaguzi wake ifikapo Juni 5 kulingana na agizo lilikotolewa na BMT na wizara.

Akizungumza na waandishi wa habari, mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi TFF, Aloyce Komba amesema mchakato mzima wa uchaguzi wa Yanga utakuwa ndani ya siku 33.

Komba ambaye pia ni Wakili, amesema mchakato rasmi wa uchaguzi wa Yanga utaanza Mei 3, 2016, Komba amesema jukumu lao TFF kusimamia na kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika hali ya demokrasia.

Wakili Komba ameongeza kuwa kamati yake itatangaza mchakato mzima wa uchaguzi huo wa Yanga na kubandika tangazo kwenye mbao za matangazo na kutangaza nafasi zitakazogombaniwa.

Mei 4-9, 2016 kuchukua fomuza wagombea na mwisho wa kurudisha kwa wagombea, Mei 10, 2016 kamati ya uchaguzi TFF itakaa kikao cha mchujo wa awali wa wagombea na kuandika barua za kuwajulisha wagombea juu ya mchujo huo wa awali.

Mei 11, 2016 kamati ya uchaguzi ya TFF itachapisha na kubandika kwenye mbao za matangazo orodha ya awali ya wagombea, Mei 12-13_ 2016 kipindi cha kupokea na kuweka pingamizi kwa wagombea wote.

Mei 14-15, 2016 kamati ya uchaguzi TFF itapitia pingamizi zote na kufanya usajili wa wagombea, Mei 16, 2016 kamati ya uchaguzi TFF itatangaza na kubandika kwenye mbao za matangazo matokeo ya awali ya usahili.

Mei 17, 2016 Sekretalieti kuwasilisha masuala ya kimaadili kwenye kamati ya maadili ya TFF, Mei 18-19, 2016 kamati ya maadili ya TFF itappkea na kusikiliza na kutolea maamuzi ya kamati maadili.

Ratiba kamili ya uchaguzi inaonyesha kuwa Mei 20, 2016 kamati ya maadili itatangaza maamuzi ya masuala ya kimaadili, Mei 21-22 kipindi cha kukata rufaa, Mei 23, kamati ya maadili TFF itasikiliza rufaa.

Mei 24, kamati ya rufaa na maadili itatoa maamuzi ya rufaa, Mei 25 na 26 kipindi cha kukata rufaa kwa kamati ya uchaguzi dhidi ya kamati ya TFF, Mei 27-28 muda wa kusikiliza rufaa na Mei 29 kamati ya uchaguzi itatangaza maamuzi ya rufaa.

Mei 30 kamati ya uchaguzi itachapisha orodha ya majina ya wagombea na kubandikwa kwenye mbao za matangazo, Mei 31 na Juni 4, kipindi cha kampeni kwa wagombea na Juni 5 ni siku ya uchaguzi mkuu wa klabu ya Yanga

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC