Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: JUMA ABDUL JAFFARI, MPISHI WA GOLI LA NGOMA, WAARABU WAMZIMIA

Na Exipedito Mataruma, ALIYEKUWA MISRI.

JUMA Abdul Jaffari ukiongeza lingine Mnyamani ni jina linalochomoza kwa sasa kwenye medani ya soka hapa nchini na kwingineko.

Anacheza nafasi ya ulinzi wa pembenj hasa akimudu upande wa kulia na akisaidia kupandisha mashambulizi, Abdul amekuwa na uwezo mkubwa wa kusababisha mashambulizi na timu yake kung' ara.

Akiwa katika kikosi hicho cha mabingwa wa soka nchini Yanga Sc, Abdul ameisaidia hadi kukamata usukani wa ligi kuu na kuweka hai matumaini yake ya kutetea ubingwa wa bara.

Nyota huyo pia amekuwa mpigaji mzuri wa mipira iliyokufa kwa maaba faulo, Abdul amejaaliwa nguvu za miguu na amekuwa akipiga mashuti makali hatimaye kuifungia timu yake magoli.

Anakumbukwa kwa magoli yake ya mashuti moja dhidi ya Azam Fc, ambapo alisawazisha makosa yake baada ya kujifunga kisha akapanda na kupiga bunduki kali na kufunga la kusawazisha, katika mchezo huo timu hizo zenye ushindani zilifungana mabao 2-2.

Abdul pia akafunga bao lingine dhidi ya APR ya Rwanda mchezo wa ligi ya mabingwa uliofanyika mjini Kigali ambapo Yanga ilishinda mabao 2-1, goli lake likiisaidia kuivusha Yanga raundi ya pili ya michuano hiyo mikubwa na yenye ukwasi mkubwa wa fedha.

Nyota yake inazidi kung' ara licha kwamba kocha wa timu ya taifa, Taifa Stars Charles Boniface Mkwassa ameshindwa kumuona, Mkwassa amekuwa akimtumia zaidi Shomari Kapombe.

Lakini Abdul ni mmoja kati ya wachezaji bora kwa sasa Afrika mashariki, beki huyo amekuwa katika kiwango cha juu mno na kuipa nguvu Yanga, Abdul alisajiliwa na Yanga misimu mitatu iliyopita akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro ambayo yenyewe ilimchukua toka Toto Africans ya Mwanza.

Tayari beki huyo ameshampoteza kabisa Mnyarwanda Mbuyu Twite ambaye alikuwa akianzishwa namba mbili, kasi ya Abdul imemfanya kocha wa Yanga Mholanzi Hans Van der Pluijm kumchezesha namba sita au tano.

WAARABU WAMTAMANI

Juma Abdul aliwashangaza Waarabu hasa wakati timu yake ya Yanga ilipocheza na Al Ahly mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa barani Afrika hatua ya 16 bora uliofanyika uwanja wa Borg Al Arab mjini Alexandria.

Kwa bahati nzuri niliushuhudia kwa macho yangu kwa maana nilikuwepo uwanjani, Abdul ndiye mpishi wa bao la Yanga walilokipata dakika ya 57 lililofungwa na Mzimbabwe Donald Ngoma, lilikuwa goli zuri lakini lilitokana na jitihada binafsi za Abdul.

Mara baada ya kumalizika mchezo huo, mashabiki wa soka nchini Misri walifurahishwa naye huku wengine wakizitaka timu za Misri kumchukua.

Abdul alizaliwa Novemba 10 mwaka 1992 mjini Mwananyamala Dar es Salaam  na kuanza soka utotoni, nyota yake ilianza kuonekana tangia anacheza chandimu, Malengo yake ya baadaye  mara baada ya kuachana na Yanga ni kucheza soka la kulipwa ughaibuni.

Yanga wameshamuongezea mkataba mpya wa miaka miwili utakaomalizika mwaka 2018

Juma Abdul akipata maelekezo toka kwa kocha wake Hans Pluijm

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC