Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: HASSAN KABUNDA, MTOTO WA NINJA WA YANGA ANAYEING' ARISHA MWADUI FC

Na Paskal Beatus, SHINYANGA

JINA la Hassan Kabunda linaonekana kama geni masikioni mwa watu, lakini wapo wanaomkunbuka beki wa zamani wa Tukuyu Stars, Yanga Sc na timu ya taifa ya Tanzania bara Kakakuona Salum Kabunda 'Ninja' ukipenda Msudan.

Beki huyo alijulikana kwa kucheza kibabe sana uwanjani mpaka ikafikia washambuliaji kuanza kumuogopa, Hassan Kabunda ni mtoto wa Salum Kabunda, lakini iko tofauti kidogo.

Hassan Kabunda yeye ni mshambuliaji na si beki kama ilivyokuwa kwa baba yake, kijana huyu amekuwa katika kiwango kizuri na kuwa msaada mkubwa kwenye timu yake ya Mwadui Fc ya Shinyanga.

Kabunda ni mshambuliaji wa timu hiyo na anakumbukwa vizuri hasa pale alipoifungia Mwadui mabao yote mawili dhidi ya Coastal Union mchezo wa ligi kuu bara Nwadui ikishinda ikishinda mabao 2-1.

Nyota huyo aliibukia katika mashindano ya Copa Cocacola akiwa na timu ya Mkoa wa Ilala, Kabunda akiwa na ndugu yake Ally Kabunda wote washambuliaji, walitamba katika michuano hiyo na baadaye wakasajiliwa na Ashanti inayoshiriki ligi Daraja la kwanza.

Kabunda amekuwa na uwezo mkubwa wa kutengeneza mashambulizi na anapokosekana uwanjani pengo lake linaonekana dhahili, mshambuliaji huyo anaichezea Mwadui Fc ya mjini hapa anbayo inanolewa na Jamhuri Kihwelu 'Julio'.

Umuhimu wake ulionekana katika mchezo wao wa ligi kuu bara dhidi ya mabingwa watetezi Yanga Sc uliopigwa uwanja wa Taifa Dar esvSalaam ambapo Yanga ilishinda 2-1, baada ya Mwadui kumtoa Kabunda na kumwingiza mkongwe Nizar Khalfan Yanga walionekana kupata ahueni kidogo.

Alipokuwepo uwanjani Kabunda, Yanga walishindwa kulifikia lango la Mwadui na matokeo yalikuwa 1-1 kipindi cha pili, lakini mabadiliko aliyoyafanya Julio ya kumtoa Kabunda yakawafanya Yanga wapande mbele na dakika ya 87 Haruna Niyonzima akaifungia Yanga bao la pili.

Kama mwalimu wa timu ya taifa, Taifa Stars Charles Boniface Mkwassa yatamulika vizuri basi kijana huyo anaweza kuwemo kwenye kikosi chake kwani ni miongoni mwa wachezaji wanaofaa kuitumikia

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC