Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MITANANGE MIWILI FA CUP KUPIGWA LEO, NANI KUCHEZA FAINALI

Na Ikram Khamees, DAR ES SALAAM

MICHUANO ya Azam Sports Federation Cup inatarajia kuendelea jioni ya leo katika viwanja viwili tofauti hatua ya Nusu fainali ambapo timu mbili zitafuzu fainali itakayopigwa mwezi Mei mwaka huu.

Tukianzia pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa soka katika miji ya Dar es Salaam na Tanga, mabingwa watetezi wa ligi kuu bara Yanga Sc watakuwa wageni wa Coastal Union ya Tanga uwanja wa CCM Mkwakwani.

Timu hizo zinakutana leo katika michuano hiyo inayofahamika zaidi kama FA Cup, Yanga inataka kulipiza kisasi kwani ilibutuliwa mabao 2-0 na vijana hao wa Wana Mangushi, Yanga ilifungwa kwenye mchezo huo wa ligi kuu bara.

Hivyo mchezo huo utakuwa mkali ikitaka kulipiza kisasi, pia ina machungu ya kutolewa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa kufungwa jumla ya mabao 3-2 na Al Ahly ya Misri, Coastal nao kwa sasa wako vizuri hasa baada ya kupata ushindi wa mara mbili mfululizo.

Coastal iliifunga Simba Sc mabao 2-1 mchezo wa Robo fainali ya FA Cup, pia ikaifunga JKT Ruvu bao 1-0 mchezo wa ligi kuu bara hivyo leo inataka kuendeleza ubabe kwa Yanga, tusubiri nini kitatokea.

Mjini Shinyanga katika uwanja wa Mwadui Complex, wenyeji Mwadui Fc itaialika Azam Fc ambao ni klabu bingwa Afrika mashariki, timu hizo zimekamiana vya kutosha katika Nusu fainali hiyo nyingine.

Kocha wa Mwadui Fc Jamhuri Kihwelu "Julio" amejitamba kumbwaga mzungu wa Azam Stewart Hall raia wa Uingereza, Azam nayo kama Yanga ina hasira ya kutolewa kwenye kombe la Shirikisho barani Afrika, Azam ilifungwa jumla ya mabao 4-2 na Esperance ya Tunisia.

Mwadui nao wana kumbukumbu mbaya ya kupoteza mechi mbili mfululizo za ligi kuu bara hivyo mchezo wa leo utakuwa mgumu na wakusisimua

Yanga Sc je watalipa kisasi?

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC