Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MICHANO: PHILIPO NYANDINDI "O TEN", ALISAHAU MSEMO HUU, UKIMUONA KOBE JUU YA MTI UJUE KAWEKWA

Na Mkola Man, TANGA

YAP....yap....yap Michano yangu ya leo inamchana Philipo Nyandindi "O Ten" kutoka mji kasoro bahari yaani Morogoro ila safari yake kimuziki ilianzia Upanga jijini Dar es Salaam katika kundi la East Coast Team.

Lakini kabla hajatua kundi hilo, O Ten alikuwa msanii wa kujitegemea huko Morogoro na siku moja wakati msanii Inspekta Haroun akitamba na 'Mtoto wa geti kali' alivutiwa na msanii huyo jukwaani na kuamua kumleta Dar es Salaam.

Inspekta ndiyo msanii wa kwanza kurekodi studio na O Ten wimbo unaojulikana kwa jina la "Siku za Hukumu ya mwisho'. na hapo ndipo safari ya O Ten ilipoanza.

KWANINI ALIINGIA EAST COAST

O Ten alijiunga na East Coast Team baada ya kutelekezwa na Inspekta ambaye alimuahidi kumsaidia kimuziki ndipo alipotua kundi hilo lililotamba sana, mwaka 2004 alitoka na nyimbo iitwayo 'Nicheki' iliyotengenezwa vizuri na prodyuza P Funk Majani iliyompa heshima ndani ya kundi lake na nje pia.

Kisha nyota yake ikaanza kung' ara na akajipatia mashabiki wengi na kuweka historia ya kufanya shoo na wapinzani wao TMK Wanaume Family katika ukumbi wa Bilicanas, kundi la East Coast lina wasanii maarufu kama King Crazy GK, Mwana FA, Pouline Zongo, Snare, Buff G, AY na O Ten mwenyewe.

Chakusikitisha sana kabla ajapata mafanikio akaanza malumbano na msanii mwenzake Afande Sele ambaye anatoka naye Morogoro akichukua muda mrefu East Coast Team ikavunjika na hapo ndipo ukawa mwisho wake licha kwamba alikongoja kidogo kwa kutoa wimbo "Akipendacho binti".

O Ten alisahau maneno ya waswahili ambayo yalitimia yanayosema ukimkuta kobe juu ya mti usishangae ujue amepandishwa, na O Ten hakuonekana tena mpaka leo, Yap Mkola Man naachia line, tukutane Ijumaa ijayo

Philipo Nyandindi "O Ten"

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC