Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ESPERANCE YAIFURUSHA AZAM KOMBE LA SHIRIKISHO

Na Salum Fikiri Jr, TUNISIA

AZAM FC imeaga michuano ya kombe la Shirikisho la soka barani Afrika  baada ya kufungwa mabao 3-0 na wenyeji Esperance katika mchezo wa marudiano hatua ya 16 bora usiku wa leo Uwanja wa Olympique de Rades mjini Tunis.

Matokeo hayo yanaifanya Azam Fc inayomilikiwa na bilionea Said Salim Bakhressa na familia yake itolewe kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya awali kushinda 2-1 Dar es Salaam.

Ikicheza mchezo wa kujihami kwa kutumia viubgo watano na mshambuliaji mmoja tu, Nahodha John Raphael Bocco, Azam ilifanikiwa kuwabana vizuri wenyeji dakika 45 za kwanza na kumaliza bila kuruhusu bao.

Timu hiyo ya kocha Muingereza Stewart Hall ilikuwa ikifanya mashambulizi ya kushitukiza kwa kumpelekea mipira mirefu Bocco, ambaye hata hivyo alidhibitiwa, ukuta wa Azam ukifanya kazi ya ziada ya kuzuia mashambulizi ya Esperance muda mwingi wa kipindi hicho huku kipa wake Aishi Manula akiokoa michomo zaidi ya minne ya hatari langoni mwake.

Hata hivyo, bao la mapema kipindi cha pili walilopata Esperance lilitibua mipango ya Azam na kuchanganyajiwa.

Bao hilo lilifungwa na Saad Bguir dakika ya 47 kwa shuti la mpira wa adhabu umbali wa mita 19, baada ya Fakhreddine Ben Youssef kuangushwa na David Mwantika nje kidogo ya boksi.

Baada ya hilo, Azam Fc walibadilisha mfumo na wao kuanza kushambulia moja kwa moja na hapo ndipo mchezo ukaanza kuwa wa pande zote.

Hata hivyo kufunguka kwa Azam kuiipa nafasi Esperance na kufanikisha mipango yake na kuongeza mabao mengine mawili yaliyopatikana dakika ya 63 na 80 yakifungwa na Haithem Jouini na na Fakhreddine Ben Youssef tena.

Pengo la kuwakosa wachezaji wake wanne Shomari Kapombe, Kipre Tchetche, Paschal Wawa na Jean Bapstita Mugilaneza kuliokana dhahili kuiathili Azam kwani hawakuweza kulitia msukosuko tena lango la Esperance

Kikosi cha Esperance kimeitoa nje ya mashindano Azam Fc 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC